Jumapili, 3 Mei 2015

Floyd Mayweather amshinda Pacquiao kwa wingi wa point


Bondia wa Marekani Floyd Mayweather ameshinda pigano lililosubiri kwa wingi katika miongo kadhaa.

 Bondia huyo ambaye hajashindwa alimshinda mpinzani wake raia wa Ufilipino Manny Pacquiao kwa wingi wa pointi.

 Mashabiki wengi waliojaa katika ukumbi wa MGM Grand Garden Arena mjini Las Vegas walimzoma mara kwa mara Mayweather.

 Kote duniani wateja millioni 3 walilipa kuliona pigano hilo ambalo ndio pigano lililovutia kitita kikubwa cha fedha katika historia ya ndondi.

Tiketi nyingi za pigano hilo ziliuzwa katika bei ya makumi ya maelfu ya dola.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni