Jumanne, 10 Desemba 2013

POLISI YAMPA ANGALIZO DK. SLAA JUU YA ZIARA YAKE MKOANI KIGOMA

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Wilbrod Slaa  
----
 Polisi mkoani Kigoma, imemshauri, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Wilbrod Slaa kusitisha ziara zake mkoani Kigoma kwa sababu za kiusalama.
 
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Zedekia Makunja alisema jana: “Ni ushauri tu tunatoa kwa Dk Slaa kwamba anaweza kuahirisha kutokana na hali ilivyo hapa.” Hata hivyo, Kamanda Makunja alisema pamoja na yote hayo bado Polisi mkoani, Kigoma imejipanga imara kukabiliana na vurugu zozote zinazoweza kutokea katika ziara hiyo.
Lakini Dk Slaa alipoulizwa kuhusu ushauri huo alisema hawezi kufuta ziara hiyo na kusema hahofii chochote. Alisema na alishafahamu siku nyingi kuwa hayo yanayotokea. Juzi, vijana mbalimbali waliandamana kwa pikipiki na wengine wakitembea kwa mguu huku wakiwa na mabango kupinga ziara ya Dk Slaa Kigoma. Anatarajiwa kuwasili Kigoma Kaskazini keshokutwa.
Hatua hiyo ya kupinga ziara hiyo, imetokana na Kamati Kuu ya Chadema kumvua madaraka aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe ambaye ni mbunge wa Kigoma Kaskazini.Kwa habari zaidi bofya na Endelea........
 

 Katibu Mkuu wa Chadema Dr Wilbrod Slaa akihutubia katika Mkutano uliofanyika  Kasulu, Kigoma  
 

  Katibu Mkuu wa Chadema Dr Wlbrod Slaa akiwa na Wananchi wa Kijiji cha Kitanga, Kigoma.Picha na Chadema


  Sehemu ya Mabango yaliyobebwa a Vijana wapatao 10-15





  


----
Pamoja na Mbinu Chafu za Kutaka Kuvuruga Mkutano wa Chadema Kasulu Uliokuwa Unahutubiwa na Dr Slaa, lakini wananchi wengi wa Kasulu walijitokeza kumsikiliza Dr Slaa na kufurahishwa na hotuba yake iliyobeba maneno ya kuwapa Matumaini. 
 
 Kulikuwa na kikundi cha Vijana wapatao kumi wenye mabango ambayo yaliandaliwa mahsusi ili yatumike kuvuruga mkutano huo lakini mbinu zao chafu zimeshindikana. Ili kuzima mipango yao michafu vijana hao walipewa fursa ya kukaa mbele na mabango yao yenye ujumbe wa kuwaponda viongozi wa Chadema.
 
 Vijana hao walipewa fursa hiyo ili kuonyesha kwamba Chadema kinaendeshwa kwa Demokrasia ya kumruhusu mwanachadema yeyote kutoa mawazo yake anayopenda ili kudumisha Demokrasia ndani ya Chama.
 
 

Jumapili, 3 Novemba 2013

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 02/11/2013

 

Imeelezwa kuwa ufaulu wa mtihani wa kumaliza darasa la saba kwa mwaka 2013 umepanda kwa masomo yote kwa asilimia 19.89 ikilinganishwa na ilivyokuwa kwa mwaka uliopita.

Kwamba, wakati mwaka jana wahitimu waliopata asilimia 100 walikuwa asilimia 30.72, mwaka huu wameongezeka kuwa asilimia 50.61. Pia, somo ambalo watahiniwa hao wamefaulu zaidi katika mtihani wao ni  Kiswahili ambapo ufaulu ni 
asilimia 69.06 huku wakiwa wamefeli zaidi kwenye somo la Hisabati ambalo ufaulu upo chini kwa asilimia 28.62.

Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Dk. Charles Msonde alisema wanafunzi 427,606 walifanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2013 huku kiwango cha udanganyifu kikizidi kudhibitiwa hivyo kupungua.

Alisema NECTA imefuta matokeo yote ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi kwa watahiniwa 13, ambao walibainika kufanya udanganyifu kwenye mtihani au kurudia pasipo ruhusa ya Baraza. Watahiniwa waliofutiwa mwaka jana ni 293.

Alisema kati ya wanafunzi hao, 844,938 waliofanya mtihani huo wamepata alama zaidi ya 100 katika alama 250: “Idadi hiyo ni sawa na asilimia 50.61. Kati yao wasichana walikuwa 208,227 (sawa na asilimia 46.68) na wavulana 219,379 sawa na asilimia 55.01,” alisema.

Dk. Msonde alisema katika ufanyaji wa mtihani huo, pia walikuwepo watu wenye ulemavu, ambapo wasichana walikuwa 219 na wavulana 257.

Alisema matokeo hayo yatapelekwa maeneo yote husika ili mchakato wa upangaji shule ukifanyika kwa watahiniwa wote waliofaulu mtihani huo wa kumaliza elimu ya msingi.

Kuhusu usahihishaji mitihani, Dk. Msonde alisema ili kujiridhisha na usahihi wa zoezi la usahihishaji wa kutumia mfumo wa kompyuta (Optical Mark Reader - OMR), sampuli za karatasi 20,795 za majibu ya watahiniwa wa shule 200 kutoka wilaya 48 zilichukuliwa kutoka shule za mikoa tisa ya (Iringa, Kagera, Shinyanga, Manyara, Njombe, Mbeya, Morogoro, Katavi na Tanga) na kusahihishwa kwa mkono: “Ulinganifu baina ya alama za watahiniwa zilizopatikana kwa kusahihishwa kwa mkono na zile zilizotokana na usahihishaji wa mfumo wa kompyuta ulifanyika na kubaini kompyuta ilikuwa sahihi,”alisema.

Amesema makosa yaliyojitokeza katika karatasi zilizosahihishwa kwa mkono ni kuweka pata pale ambapo kuna kosa ama kuweka kosa pale ambapo kuna pata, makosa ambayo kwenye usahihishaji wa kutumia kompyuta hakuwepo.

Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Shule na Vyuo Binafsi Tanzania (TAMONGSCO), Mahmoud Mringo alisema shule binafsi zimeongoza katika matokeo hayo kwa kila somo.

Alisema katika somo la Kiswahili, shule binafsi wamepata asilimia 98 wakati za Serikali asilimia 68, na kwa Kingereza shule binafsi asilimia 99 na Serikali 33. Kwa somo la Maarifa ya Jamii, shule binafsi asilimia 86 Serikali 52 , Hisabati shule binafsi asilimia 81 na Serikali 27 na somo la Sayansi, shule binafsi asilimia 84 na Serikali 46.

Matokeo ya dalasa la saba yaliyopachikwa hapo juu pia yanapatikana katika tovuti za:

  1. www.necta.go.tz
  2. www.edu.udsm.ac.tz
  3. www.matokeo.necta.go.tz
  4. www.moe.go.tz



Alhamisi, 31 Oktoba 2013

MWILI WA TIGER MWAIGOMOLE AFIA MAHAKAMANI AKISUBIRI KUMWEKEA DHAMANA MWANAYE TUKUYU

Tiger Mwaigomole (70) Mkazi wa kata ya Masukulu wilayani Rungwe amefariki dunia ghafla akiwa katika chumba cha Mahakama ya Wilaya ya Rungwe akifuatilia mwenendo wa kesi inayomkabili mtoto wake wakati Mahakama ikiendelea.




MTU mmoja aliyefahamika kwa jina la Tiger Mwaigomole (70) Mkazi wa kata ya Masukulu wilayani Rungwe amefariki dunia ghafla akiwa katika chumba cha Mahakama ya Wilaya ya Rungwe akifuatilia mwenendo wa kesi inayomkabili mtoto wake wakati Mahakama ikiendelea.
Tukio hilo la aina yake lilitokea hivi karibuni majira ya saa 9 alasiri ndani ya Mahakama hiyo ambapo Marehemu alifika mahakamani hapo akiwa na mwanaye aliyejulikana kwa jina la Lusajo Tiger (40) wakiwa na lengo la kumwekea dhamana ndugu yao Gwakisa Tiger ambaye alifikishwa mahakamani hapo akituhumiwa kwa kosa la kupigana na kujeruhi katika ugomvi uliotokea kijijini kwao.
Kwa mujibu wa mtoto wa Marehemu aliyekuwa ameongozana nae Mahakamani hapo Lusajo Tiger alisema wakati kesi ikiendelea chini ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Rungwe, Kingwele, ndugu yao alipandishwa kizimbani kusomewa mashtaka yanayomkabili ndipo marehemu alipoanza kutetemeka kwa madai kuwa anajisikia baridi kali sana.
Alisema kutokana na marehemu kulalamikia baridi aliamua kumnunulia chai ya moto ili anywe na kupunguza baridi ambapo baada ya kufanya hivyo marehemu alikata roho muda mfupi baada ya kumaliza kunywa chai aliyokuwa amepelekewa huku akiwa amekaa ndani ya chumba cha mahakama hiyo.
Kutokana na tukio hilo Askari polisi waliokuwepo mahakamani hapo waliuchukua mwili wa marehemu na kuukimbiza katika Hospitali ya Wilaya ya Rungwe Makandana kwa ajili ya vipimo lakini hata hivyo mwili ulikabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya taratibu za mazishi ingawa ripoti ya kifo chake haikutolewa mapema.
Wakati huo huo Hukumu ya kesi ya mauaji dhidi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Rungwe, John Mwankenja inayowakabili Hakimu Mwakalinga na wenzie watatu huenda ikatolewa Novemba 11 mwaka huu baada ya Mahakama kuu kanda ya Mbeya chini ya Jaji Samwel Karua kumaliza kusikiliza ushahidi wa upande wa mashtaka pamoja na utetezi kwa upande wa watuhumiwa.
Kwa mujibu wa Jaji Karua alisema baada ya kumaliza kusikiliza pande zote mbili atatumia muda wa siku mbili kwa ajili ya kuandika hukumu ambayo itaitoa Novemba 11, Mwaka huu, kesi ambayo inasimamiwa na Mwanasheria wa Serikali Archiles Mulisa huku watuhumiwa wakitetewa na Mawakili wawili wa kujitegemea ambao ni Simon Mwakolo na Victor Mkumbe.

Na Mbeya yetu

Jumatano, 30 Oktoba 2013

BREAKING NEWS LIVE MUDA HUU: MTOTO JOSHUA ISACK MIAKA 4 ALIEPOTEA AKIWA ANACHEZA NA WATOTOWENZAKE JUZI AKUTWA AMEFARIKI NDANI YA SHIMO LA CHOO CHA JIRANI.

 Huu ni Mwili wa Marehemu Joshua Isack Miaka 4 baada ya kutolewa Chooni.


 Wananchi wakiwa katika hali ya majonzi mazito sana.


Picha kamili na Habari Kesho.. endelea kufuatilia 

Picha na Mbeya yetu Blog


RUFAA YA BABU SEYA, PAPII KOCHA KILICHOBAKI NI HUKUMU TU

 Nguza Viking ‘Babu Seya’ (wa pili kulia) na mwanaye Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ (wa pili kushoto) wakiwa mahakamani.


Nguza Viking ‘Babu Seya’ (kulia) na mwanaye Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ wakitoka mahakamani kwa furaha.

 ......................................................

Baada ya majaji wa Mahakama ya Rufaa jijini Dar es Salaam kupitia hoja za mawakili wa serikali na utetezi kwenye Rufaa ya hukumu ya kifungo cha maisha jela katika kesi iliyokuwa ikimkabili mwanamuziki Nguza Viking ‘Babu Seya’ na mwanaye Johnson Nguza ‘Papii Kocha’, wameamua kuhairisha rufaa hiyo mpaka tarehe husika ya kutoa hukumu ya kesi hiyo itakapopangwa hapo baadaye.

(Picha na Richard Bukos / GPL)

 

Alhamisi, 24 Oktoba 2013

Uswisi sasa kurejesha mabilioni ya mafisadi

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (katikati) akiwa na maafisa wa Serikali ya Uswis pamoja na timu uchunguzi kufuatilia mabilioni ya fedha zilizowekwa katika benki za nchi hiyo. 

Picha na Bernhard Reinhold.

  ........................................................................

Dar es Salaam. Sakata la vigogo kuficha mabilioni ya shilingi katika benki za Uswisi, limechukua sura mpya baada ya Serikali ya nchi hiyo kutunga sheria inayowabana walioweka fedha kwenye benki zake kuzithibitisha, la sivyo zitarejeshwa katika nchi husika.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe alifanya mazungumzo na Serikali ya nchi hiyo ambayo imemweleza kuwa imebadili sheria zake ili kuwadhibiti wageni wanaoficha fedha nchini humo.

Akizungumza na gazeti hili, Zitto alisema amepata taarifa hizo juzi baada ya kukutana na Waziri wa Fedha wa nchi hiyo ambaye alimwandalia mazungumzo na watalaamu wake.

Alibainisha kuwa tangu kuibuka kwa sakata hilo mwaka 2012 na Bunge kuiagiza Serikali kufuatilia, Serikali haijaomba taarifa yeyote kutoka Uswisi kuhusu Watanzania waliohifadhi fedha nchini humo.

“Jana nilikutana na Waziri wa Fedha na akatuacha na mazungumzo na wataalamu wake. Wamesema hadi sasa, Tanzania haijasaini mkataba wa kubadilishana taarifa za kikodi (Multilateral convention on administrative assistance in tax matters),” alisema Zitto na kuongeza;

“Kwa kutosaini, Tanzania inajinyima haki ya kupata taarifa hizi na kutoza kodi kwa watu walioficha fedha huku (Uswisi), maana Sheria ya Kodi ya Tanzania inataka kila Mtanzania popote anapopata kipato halali lazima alipe kodi.”

Zitto alieleza kuwa kitendo cha Serikali ya Uswisi kubadili sheria zake, kinaiwezesha nchi hiyo kutoa taarifa za benki za watu walioweka fedha nchini humo wakiwamo Watanzania, ambao sasa watatakiwa kuthibitisha kama fedha hizo ni safi au la.

“Kiufupi, Tanzania haijaomba taarifa yeyote kutoka Uswisi. Ila Uswisi wamebadili sheria yao na sasa mmiliki wa fedha ndiyo anapaswa kuthibitisha kwamba ni safi, na ikithibitika kuwa hazina mwenyewe wala maelezo, zitarudishwa nchi husika,” alisema.

Zitto alisema mbali na kukutana na watendaji hao wa Serikali amezungumza na Umoja wa Mabenki wa nchi hiyo uliobainisha kuwa Uswisi ina Watanzania wachache wenye fedha.

“Wamesema Watanzania wengi wana fedha Uingereza, Jersey, Cayman Islands na Mauritius. Dubai pia imetajwa sana,” alisema Zitto. Zitto alielezea kuwa umoja huo wa benki za Uswisi umeanzisha mkakati wa kusafisha fedha uitwao ‘clean money strategy’, na wamegundua watu wengi ambao ni wanasiasa, wamezuia akaunti zao na kupeleka majina kwenye Serikali zao.

“Tanzania haijafanya maombi rasmi hapa Uswisi na hivyo wao kama benki hawawezi tu kutoa taarifa bila kuombwa. Sheria yao imerekebishwa ambapo sasa ni wajibu wa mwenye akaunti kusema kama fedha zake ni halali au hapana,” alisema Zitto na kuongeza.

Hivi sasa hawapokei pesa kutoka nchi za Afrika au wanapokea kwa tahadhari sana, maana kuna reputational risk (kupoteza heshima),” alisema.

1 | 2 | 3 Next Page»

 

Jumatatu, 21 Oktoba 2013

HATARIIII RELI YA TAZARA YAZIDI KUHUJUMIWA NAWAUZA VYUMA CHAKAVU MKOANI MBEYA



 

HIZI NI BAADHI YA RELI ZILIZOFUNGULIWA BOLTI 






HILI NI ENEO LA MLIMA MBALIZI SEHEMU HII RELI IENDAYO ZAMBIA IMEPITA JUU YA DARAJA. 


 WATU WAKISHANGAA KUONA JINSI RELI ZILIVYOFUNGULIWA NA HUDUMA ZA TRENI ZIKIENDELEA KAMA KAWAIDA




Picha Na Ezekiel Kamanga
Mbeya yetu

Jumamosi, 19 Oktoba 2013

SEBA ERNEST MWAKASULA[45] ameuawa kwa kukatwa kichwani na tumboni na vitu vyenye ncha kali na mtu au watu wasiofahamika kisha mwili wake kutupwa mita chache kutoka nyumbani kwake. wilayani Mbarali

 Baadhi ya majirani wakiwa jirani na mwili wa marehemu Seba wakisubiri polisi kuja kuuchukua mwili huo

MWILI WA MAREHEMU SEBA UKIWA UMEFUNIKWA

 


NDUGU WA MAREHEMU WAKIWA WANAOMBOLEZA WAKATI WAKIWASUBILI POLISI



SEBA ERNEST MWAKASULA[45] ameuawa  kwa kukatwa kichwani na  tumboni na vitu vyenye ncha kali  na mtu au watu wasiofahamika kisha mwili wake kutupwa mita chache kutoka nyumbani kwake.

Mke wa marehemu JOYCE DANIEL[39]amesema waliagana na marehemu majira saa mbili usiku akimtaarifu kuwa asubuhi ya octoba 19 mwaka huu atasafiri kuelekea Wilaya ya CHUNYA kwa ajili ya kujenga makaburi.

Aidha imedaiwa baada ya kutoka nyumbani kwa mke mdogo marehemu alipita kilabuni ambapo watu kadhaa walimwona marehemu akipata viburudisho.

Baadhi ya majirani wamesema kuwa hawakusikia sauti yoyote ya mtu kuomba msaada ingawa ni karibu na makazi ya watu hali inayosadikika mauaji kufanywa eneo jingine na mwili kutupwa karibu na nyumbani kwake

Mwenyekiti wa kijiji cha NSONYANGA ASUMILE MTAWA amesema alipata taarifa kutoka kwa mtendaji wa kijiji ambapo walifika eneo la tukio na kukuta marehemu amekatwa kichwani na utumbo ukiwa nje.

Diwani wa kata ya Mahongole BROWN MWAKIBETE amesema kuwa kitendo kilichofanywa na wauaji hao ni cha kinyama ambapo amewataka wananchi kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi li watuhumiwa wakamatwe ili kujibu tuhuma za mauaji.

Mwili wa marehemu ulifanyiwa uchunguzi na Daktari kisha kukabidhiwa kwa ndugu wa marehemu kwa mazishi.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya DIWANI ATHUMANI amethibitisha kutokea kwa kifo hicho na kutoa wito kwa mtu au watu wanaowafahamu wliohusika na tukio hilo watoe taarifa polisi il wakamatwe na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Picha na Ezekiel Kamanga
Mbeya yetu

Jumatatu, 14 Oktoba 2013

MWANDISHI WA ITV / RADIO ONE UFOO SARO APIGWA RISASI, NA MCHIMBA WAKE NA MAMA YAKE AUAWA PAPO HAPO.

Rais Kikwete (kushoto) akipeana mkono na Ufoo Saro, alipokutana na Waandishi na Wahariri wa Vyombo mbalimbali vya Habari Ikulu jijini Dar es Salaam Desemba 2012. (picha: Bayana blog)

 

Mtu mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Bwana Anthery Mushi, amempiga risasi Mwandishi wa Habari wa ITV/Radio One , Ufoo Saro na kumjeruhi vibaya.

Aidha Anthery Mushi amempiga risasi kumuua mama yake mzazi Ufoo Saro na kisha kujiua, katika tukio lililotokea leo asubuhi maeneo ya Kibamba CCM, Wilayani Kinondoni Jijini Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi wa Kanda ya Kinondoni, Bwana Camilius Wambura amesema tukio hilo limetokea saa 12 na nusu leo asubuhi na kusema inadaiwa kuwa Anthery Mushi ni mume au mchumba wa Ufoo Saro anafanya kazi Umoja wa Mataifa na kituo chake cha kazi ni nchini Sudan.

Kamanda Wambura amesema Anthery Mushi alirejea jana kutoka Sudan na leo majira ya saa 12 waliondoka yeye na Ufoo Saro wakitokea eneo la Magari Saba kwenda kwa Mamake Ufoo Saro, Kibamba CCM.

Amesema kilichoendelea huko bado askari wanaendelea na uchunguzi, lakini taarifa zinasema walipofika huko Anthery Mushi alichukua bastola na kumpiga risasi kifuani mama mzazi wa Ufoo Saro na na kisha kumpiga Ufoo risasi tumboni na mguuni kisha yeye kujipiga risasi juu ya kidevu na kufariki dunia papo hapo.

Ufoo Saro alikimbizwa Hospitali ya Taifa Muhimbili ambako anapatiwa matibabu na hali yake inaendelea vizuri.
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dakta Reginald Mengi, amefika katika hosptiali hiyo kumjuilia hali Ufoo Saro.

CHANZO: RADIO ONE

HIZI NI BAADHI YA PICHA WAKATI ANAFANYIWA OPARESHENI 


 ufo saro akiwa katika chumba cha upasuaji baada ya kutolewa risasi sehemu mbalimbali za mwili wake


 waandishi wa habari wakimpiga picha ufo saro baada ya kutolewa chumba cha upasuaji

  WAANDASHI WA HABARI KUTOKA VYOMBO MBALIMBALI  WAKIMSINDIKIZA UFO SARO AKIPELEKWA WODINI.

                               PICHA NA MWAIBALE




HATARI SANA: MWANDISHI WA HABARI MJINI TUNDUMA AVAMIWA NA MAJAMBAZI NA KUPIGWA RISASI, AJERUHIWA VIBAYA.

NDUGU SHOMI MTAKI AKIWA KATIKA MASIKITIKO MAKUBWA NI BAADA YA KUVAMIWA NA MAJAMBAZI NA KUMSABABISHIA JERAHA KUBWA KATIKA MGUU WAKE WA KUSHOTO

N

Jeraha katika mguu wa mwandishi wa habari Shomi Mtaki lililotokana na risasi baada ya kuvamiwa na majambazi.

 

 Shomi Mtaki akionesha jeraha lililotokana na risasi katika mguu wake wa kushoto

 Mwandishi wa habari wa ITV/Radio One wilayani Mbozi Danny Tweve alipomtembelea Shomi Mtaki kumjulia hali baada ya kuvamiwa na majambazi na kujeruhiwa kwa risasi





 
Sehemu ambayo risasi ilipigwa katika mlango






 Namna ambavyo majambazi yalivyofanya upekuzi katika chumba cha Mtaki kutafuta fedha walizodhani kuwa amehifadhi

 Mke wa Shomi Mtaki ambaye naye alijeruhiwa na baruti kifuani kwake






 Ndugu na jamaa wakiifariji familia ya Mtaki baada ya tukio hilo la uvamizi na kupigwa risasi






 

Kamanda wa Polisi wilaya ya Momba Bw. Chitanda akimpa pole Shomi Mtaki

 



 HAPA NDIO ENEO LA TUKIO HILO TRECTA NA NYUMBA NI MALI YA SHOMI MTAKI (SHAMBANI KWAKE)

NI wiki ya majanga kwa waandishi wa habari nchini, muda mfupi baada ya kupata taarifa ya kupigwa risasi kwa Mwandishi wa habari wa ITV /Radio One Mwandishi mwingine wa gazeti la Uhuru mjini Tunduma  wilayani Momba mkoani Mbeya  Shomi Mtaki amepigwa risasi baada ya kuvamiwa na majambazi shambani kwake katika mji mdogo wa Mpemba.
Mtaki ambaye alikuwa katika nyumba iliyopo shambani kwake alivamiwa usiku wa Octoba 10 na watu watano waliokuwa na silaha aina ya bunduki kisha kumlazimisha kutoa fedha.
Wanablogu waliomtembelea shambani kwake walishuhudia majeraha aliyokuwa nayo Mtaki katika maeneo mbalimbali ya mwili wake ambapo alisema kuwa siku hiyo majira ya saa 9:00 usiku alisikia mchakato wa miguu nje ya nyumba yake na kwamba alipochungulia aliwaona vivuli vya watu wakiwa wamesimama karibu na trekta lake nje ya nyumba.
Alisema kuwa alipowashitua watu hao walitamka wazi wazi kuwa wanataka fedha na muda huo huo akasikia kishindo kikubwa katika mlango wa kuingilia sebuleni ambapo wavamizi hao walikuwa wamepiga jiwe aina ya FATUMA kwa lengo la kuuvunja mlango ili waingie ndani.
Alisema kuwa mara akasikia mlio wa risasi ikipigwa katika mlango wake na mara ukafunguka na vijana watatu waliingia sebuleni ambapo walichukua jiwe walilotumia kuvunja mlango wa sebuleni na kupiga katika mlango wa chumbani na kisha baadaye walimimina risasi katika mlango huo ambazo zilimpata katika mguu wa kushoto na kumjeruhi.
Mtaki alisema kuwa yeye na mkewe walikuwa wakihangaika na kujaribu kujiokoa maisha yao ambapo mkewe aliposikia mlio wa risasi aliingia chini ya mvungu wa kitanda ili kujinusuru.
‘’Nilijiona nakikaribia kifo vijana walimimina risasi katika mlango wa chumbani zikanikuta mguuni na kunijeruhi vibaya, mlango ukafunguka wakaingia vijana watatu ambao hawakujiziba sura zao,’’alisema.
Alisema kuwa mara baada ya kuingia walianza kumuamrisha atoe fedha, akawajibu kuwa hana fedha ndipo walipoanza kumpiga mgongoni huku wakitishia kumuua na kwamba wakati huo mkewe alikuwa amejificha katika mvungu wa kitanda.
‘’Wale wavamizi walianza kupekuwa vitu mbalimbali, wakachukua simu yangu ya mkononi ambayo mtu wa mwisho kuwasiliana naye alikuwa ni shemeji yangu ambaye ni Mwanajeshi,’’alisema na kuongeza.
‘’Wavamizi wale walichukua simu tatu, simu moja ikajipiga kwa bahati shemeji yangu aliipokea, akasikia vurumai iliyokuwa ikiendelea nyumbani na namna ambavyo tulivyokuwa tukijitetea ili tusiuawe, muda huo huo akaenda kutoa taarifa polisi,’’alisema.
Alisema kuwa wavamizi hao waliingia katika mji wake majira ya saa 8:45 na kuendelea kuwepo pale hadi majira ya saa 9;00 usiku ambapo walichukua simu tatu, tv seat ya nchi 22, ving’amuzi viwili kimoja cha Startimes na kingine cha Zuku vyote vikiwa na thamani ya sh. Milioni 2.
Alisema kuwa mara baada ya wavamizi hao kumaliza kukusanya vitu walivyoona vinafaa waliwaamrisha kuingia chumbani na wao wakatokomea upande wa mashariki na muda mfupi baadaye polisi walifika eneo la tukio wakatukuta mien a mke wangu tukiwa tumekumbatiana huku tukilia na kumuomba Mungu.
 
PICHA NA HABARI NA. MBEYA YETU.