Alhamisi, 28 Januari 2016

Rais Dkt Magufuli Afanya Uteuzi Wa Naibu Gavana Wa Benki Kuu Ya Tanzania


Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, amemteua Ndugu Julian Banzi Raphael, kuwa Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania.

Kabla ya uteuzi huu Ndugu Julian Banzi Raphael alikuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Biashara na Viwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.


Ndugu Julian Banzi Raphael anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Ndugu Juma RELI ambaye muda wake umemalizika tarehe 12 Julai, 2015.

Jumanne, 19 Januari 2016

Mwanamke Akutwa Kwenye Paa La Jengo La Wizara Ya Fedha Na Mipango Jijini Dar Es Salaam Leo.

Mwanamke Akutwa Kwenye Paa La Jengo La Wizara Ya Fedha Na Mipango Jijini Dar Es Salaam Leo.


Manamke ambaye jina lake halikupatikana mara moja akiwa amekaa juu ya paa la majengo ya Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dar es Salaam leo.


Mwanamke huyo akizungumza na watu waliokusanyika lakini alikuwa hasikiki vizuri maneno aliyokua akiongea kutokana na wananchi waliokusanyika kumuuliza maswali mengi kwa wakati mmoja. 
 

Polisi akiwa pembeni ya uzio wa majengo ya wizara ya fedha na mipango mara baada ya mwanamke huyo kuwa juu ya paa la nyumba hizo. Baada ya muda wafanyakazi wa wizara hiyo walimwekea ngazi na kumshusha ili kumhoji zaidi nini kimemfanya apande juu ya paa la majengo hayo.

Jumamosi, 9 Januari 2016

Rais Benjamin Mkapa Naye Ataka Kutumbua Majipu, Amwambia Rais Magufuli Haya Hapa..


RAIS mstaafu Benjamin Mkapa, amesema yuko tayari kutoa ushirikiano wa kila aina au kufanya kazi yoyote endapo Rais Dk. John Magufuli atahitaji.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa, ilisema Mkapa alitoa kauli hiyo baada ya kukutana na kufanya mazungumzo Ikulu na Rais Magufuli.

Ilisema lengo la Mkapa kukutana na Rais Magufuli ni kumpongeza kwa dhamana aliyopewa na Watanzania kuiongoza nchi, kuunda Serikali na kumtakia heri ya mwaka mpya.

Mkapa amemhakikishia Rais Magufuli kuwa yupo tayari kutoa ushirikiano wakati wote ama kufanya kazi yoyote endapo atahitajika kufanya hivyo,” ilisema taarifa hiyo.

Pia Rais Magufuli alikutana na Waziri Mkuu mstaafu Jaji Joseph Warioba ambaye alisema Watanzania wote wanapaswa kumuunga mkono kiongozi huyo kwa kazi kubwa anazofanya ambazo ni kukomesha rushwa, ufisadi, matumizi mabaya ya madaraka na wizi wa mali za umma.

Lazima kila mmoja amuunge mkono Rais, tusije tukamuachia, pale ulipo kama ni mambo ya rushwa uanzie hapo hapo, mambo ya matumizi mabaya ya madaraka anzia hapohapo, tusije tukamuachia Rais peke yake… yeye awe kiongozi wetu, lakini Watanzania wote tushughulike na matatizo hayo,” ilisema taarifa hiyo ikimkariri Jaji Warioba.

Pamoja na kumtakia heri ya mwaka mpya, Jaji Warioba alimpongeza Rais Magufuli kwa jinsi alivyoanza kazi vizuri, hususani katika kusimamia ukusanyaji wa mapato, kubana matumizi na kuelekeza matumizi kwenye maeneo muhimu ambayo yanawahusu wananchi ikiwamo afya na maji.
Kauli ya Mkapa na Jaji Warioba imekuja siku moja tu baada ya juzi Rais mstaafu Jakaya Kikwete kumtembelea Rais Magufuli Ikulu na kufanya naye mazungumzo ambayo hata hivyo yameendelea kuwa ni siri.

Hii ni mara ya kwanza kwa viongozi wastaafu ndani ya siku mbili kumtembelea Rais Magufuli tangu ameingia Ikulu Novemba 5, mwaka jana.