Alhamisi, 30 Julai 2015

PICHA: Lowassa Achukua Fomu ya Urais CHADEMA


Edward Lowassa akionesha fomu ya kuwania urais aliyokabidhiwa leo Makao makuu ya Chadema,D ar.
CLJ5hSGWoAACCU3
Umati wa watu waliojitokeza kumpokea Lowassa wakati akichukua fomu ya urais kupitia Chadema.
CLJ8fhkW8AA6IKB
…Akisaini katika kitabu cha wageni.
CLJ9y4iWEAAZWy7
Mnadhimu Mkuu kambi rasmi ya upinzani bungeni, Tundu Lissu akitoa yake machache.CLJ52JsWwAA--Yc
Lowassa akiwasiri kwenye Ofisi za Makao Makuu ya Chadema, Dar leo.
CLKRw2sWcAAzeL9
Baada ya kuchukua fomu.
mbowe na lowassa
Mwenyekiti wa Chadema (kushoto) Mhe. Freeman Mbowe Mhe. Edward Lowassa (katikati) wakati wa zoezi la kuchukua fomu lililofanyika leo Makao Makuu ya Chadema Kinondoni jijini Dar .
LOWASA (1)
LOWASA (2)
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa akiwa katika meza kuu ya Chadema.
 **
WAZIRI MKUU wa zamani, Mhe. Edward Lowassa hivi punde amechukua fomu ya kuwania nafasi ya urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
 
Lowassa amekabidhiwa fomu hiyo na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe kwenye ofisi za Makao Makuu ya chama hicho yaliyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam.
 
Lowassa alijiunga rasmi na Chadema juzi akitokea CCM baada ya kuondolewa kwenye mchakato wa kuwa mgombea urais wa chama hicho akidai kuwa jina lake liliondolewa kwa mizengwe.

Jumatano, 29 Julai 2015

Job Ndungai amshushia kipigo mgombea mwenza.

Mtia nia wa Jimbo la Kongwa, Dk. Joseph Chilongani akiwa amelazwa hospitali mjini Kongwa
 Mtia nia wa Jimbo la Kongwa, Dk. Joseph Chilongani akiwa amelazwa hospitali mjini Kongwa


NAIBU Spika na Mbunge wa Jimbo la Kongwa Job Ndugai amemshushia kipigo mgombea mwenzake Dk.Joseph Chilongani na kusababishwa kuzirai na kukimbizwa katika hospitali ya Wilaya ya Kongwa. Anaandika Dany Tibason, Kongwa, Dodoma … (endelea).
Ndugai alimpiga kwa fimbo Dk. Chilongani kutokana na kitendo chake cha kutumia simu yake ya mkononi kurekodi matukio ya ubishani baina yao na Saimon Ngatunga.
Akizungumza na gazeti hili, mdogo wa mgombea huyo Michael Chilongani alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 10 jioni katika Kata ya Ugogoni mjini Kongwa wakati wakiwa kwenye kampeni ya kujinadi kwa wanachama.
Amesema ndugu yake huyo amepigwa fimbo kichwani na tumboni na kusababisha kupoteza fahamu kwa zaidi ya saa mbili ambapo alikimbizwa kituo cha polisi kwa ajili ya kupatiwa fomu namba tatu na kisha kupelekwa hospitali.
Ndugai alimshushia kipigo mwenzake baada baada ya mgombea aliyetangulia kudai kwamba iwapo Chama kitampa ridhaa ya kuwania nafasi ya ubunge hatahakikisha anapambana ubadhirifu wa fedha katika halmashauri.
‘Baada ya fahamu kumrudia majira ya saa moja na nusu usiku, kaka alidai anasikia maumivu makali kwenye paji la uso pamoja na kichwani huku akipata shida kuzungumza,’ amesema.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo waliliambia gazeti hili kuwa kabla ya Dk. Chilongani kujeruhiwa kwa fimbo na mgombea mwenzake alitaka kumpiga fimbo hiyo mgombea mwingine aliyejinadi kuwa atakomesha ubadhirifu katika halmashauri ambapo kamati ya ulinzi iliwahi kumzuia.
Naye Kaimu Katibu wa CCM wilaya ya Kongwa Peter Minja amesema kila mgombea ambaye anamalalamiko ayapeleke katika vikao husika.
Kuhusu vurugu za ndugai kumpiga mwenzake amesema mpaka sasa hawajapokea malalamiko yoyote kwa utaratibu unaotakiwa na badala yake wamekuwa wakipokea malalamiko ya maneno.
Alipotafuwa Mkuu wa polisi Mkoa wa Dodoma David Misime alipotakiwa kuzungumzia suala hilo kama amepokea taarifa za Ndugai kumpiga mwenzake amesema hana taarifa .
Amesema hayupo ofisini na akiwa ofisini na kupata taarifa ataweza kuviarifu vyombo vya habari.
NAIBU Spika na Mbunge wa Jimbo la Kongwa Job Ndugai amemshushia kipigo mgombea mwenzake Dk.Joseph Chilongani na kusababishwa kuzirai na kukimbizwa katika hospitali ya Wilaya ya Kongwa.
Ndugai alimpiga kwa fimbo Dk.Chilongani kutokana na kitendo chake cha kutumia simu yake ya mkononi kurekodi matukio ya ubishani baina yao na Saimon Ngatunga.
Akizungumza na gazeti hili, mdogo wa mgombea huyo Michael Chilongani alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 10 jioni katika Kata ya Ugogoni mjini Kongwa wakati wakiwa kwenye kampeni ya kujinadi kwa wanachama.
Amesema ndugu yake huyo amepigwa fimbo kichwani na tumboni na kusababisha kupoteza fahamu kwa zaidi ya saa mbili ambapo alikimbizwa kituo cha polisi kwa ajili ya kupatiwa fomu namba tatu na kisha kupelekwa hospitali.
Ndugai alimshushia kipigo mwenzake baada baada ya mgombea aliyetangulia kudai kwamba iwapo Chama kitampa ridhaa ya kuwania nafasi ya ubunge hatahakikisha anapambana ubadhirifu wa fedha katika halmashauri.
‘Baada ya fahamu kumrudia majira ya saa moja na nusu usiku, kaka alidai anasikia maumivu makali kwenye paji la uso pamoja na kichwani huku akipata shida kuzungumza,’ amesema.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo waliliambia gazeti hili kuwa kabla ya Dk. Chilongani kujeruhiwa kwa fimbo na mgombea mwenzake alitaka kumpiga fimbo hiyo mgombea mwingine aliyejinadi kuwa atakomesha ubadhirifu katika halmashauri ambapo kamati ya ulinzi iliwahi kumzuia.
Naye Kaimu Katibu wa CCM wilaya ya Kongwa Peter Minja amesema kila mgombea ambaye anamalalamiko ayapeleke katika vikao husika.
Kuhusu vurugu za ndugai kumpiga mwenzake amesema mpaka sasa hawajapokea malalamiko yoyote kwa utaratibu unaotakiwa na badala yake wamekuwa wakipokea malalamiko ya maneno.
Alipotafuwa Mkuu wa polisi Mkoa wa Dodoma David Misime alipotakiwa kuzungumzia suala hilo kama amepokea taarifa za Ndugai kumpiga mwenzake amesema hana taarifa .
Amesema hayupo ofisini na akiwa ofisini na kupata taarifa ataweza kuviarifu vyombo vya habari.

Jumanne, 28 Julai 2015

CCM KUMJIBU LOWASSA LEO


Wednesday, July 29, 2015

CCM Kumjibu LOWASSA Leo


Baada ya Mbunge wa Monduli Edward Lowassa kutangaza kuhama Chama Cha Mapinduzi (CCM)  na kuhamia Chadema jana katika ukumbi wa Bahari Beachi jijini Dar es salaam, chama cha Mapinduzi kimetoa taarifa ya kuzungumza na Vyombo vya Habari  leo.
 
Taarifa hiyo ya chama cha Mapinduzi haijafafanua kuwa ajenda itakuwa nini katika kikao hicho lakini kwa mujibu wa watafiti wa masuala ya kisiasa wanasema kuwa kikao hicho kitakuwa maalumu kwa ajili ya kujibu shutuma zilizotolewa na Lowassa kuhusiana na madai ya kuwepo uonevu wakati akiomba ridhaa ya kupeperusha Bendera ya CCM.
 
Mtandao huu utakujulisha kitakachojiri katika mkutano huo.



Jumatatu, 27 Julai 2015

Lowasa ajiunga rasmi CHADEMA




BREAKING NEWS : LOWASA AJIUNGA CHADEMA RASMI, PICHA NA VIDEO ZA KILICHOONGELEWA LEO NMEKUWEKEA 

 


Lowassa Akaribishwa Rasmi UKAWA......

 

“Watanzania wanataka mabadiliko, wasipoyapata ndani ya CCM watayatafuta nje”. Hii ni moja ya kauli  ambayo Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli, Edward Ngoyai Lowassa aliziongea Arusha May 30 2015 alipotangaza nia ya Kugombea Urais kupitia CCM.
 
CCM ilikuwa na Wagombea zaidi ya 40 ambao walitangaza nia na kuchukua fomu za Kugombea Urais 2015 lakini baadae Chama hicho kikampitisha Dk. John Pombe Magufuli kugombea nafasi hiyo, baada ya hapo kukawa na  taarifa nyingi sana kuhusu ishu ya Edward Lowassa na UKAWA.
 
Viongozi wa Umoja wa UKAWA wamekutana Dar  leo  na mmoja wa Viongozi hao, James Mbatia amesema wamekubaliana kumkaribisha Mbunge Edward Lowassa ndani ya UKAWA na wako tayari kumpa nafasi na kushirikiana nae.

Mbatia  ameongeza kuwa Lowassa ni mchapa kazi makini na mfuatiliaji wa karibu wa kiutendaji katika majukumu anayokabidhiwa.
 
Alipoulizwa kuwa Lowassa atakuwa mgombea Urais Mbatia amesema kila chama kina utaratibu wake  hivyo mchakato ukishakamilika  atatangazwa mgombea urais wa UKAWA mmoja  mwanzoni mwa mwezi agosti.




 

Jumatatu, 20 Julai 2015

Majambazi Walioua Polisi na Raia Kituo cha Polisi Stakishari Wakamatwa



MAJAMBAZI waliovamia Kituo cha Stakishari jijini Dar es Salaam watatu wauwawa na wawili watiwa mbaroni wakati wakitupiana risasi katika eneo la Tuangoma, Kigamboni jijini Dar es Salaam.
 
Tukio hilo la kukamatwa na kuuawa kwa majambazi hao lilitokea Julai 17 mwaka huu huko maeneo ya Tuangoma Kigamboni jijini Dar es Salaam, na majambazi wa tukio la kinyama la kuuwawa kwa askari wanne na raia watatu katika kituo cha Stakishari wanakadiriwa kuwa kati ya 16 hadi 18. 
 
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam ,Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Kamishina Suleiman Kova amesema kukamatwa kwa majambazi hao  inatokana na kikosi kazi kilichoundwa na kanda maalumu kwa kushirikia na Mkoa Pwani.
 
Kukamatwa kwa watuhumiwa hao wa ujambazi kulitokana na taarifa pamoja na mtego wa kiintelejensia katika eneo la Tuangoma ndipo majambazi wakapita na pikipiki mbili walipowasimamisha askari majambazi hao walikaidi amri nakisha kuanza kurusha risasi na polisi wakajibu na majambazi watatu kuuwawa.
 
Majambazi waliouawa ni Abbas Hashimu Mkazi wa Mbagala,Yassin alitambulika kwa jina moja mkazi wa Kitunda Kivule, pamoja Saidi aliyetambulika kwa jina moja mkazi wa Mandimkongo ,Mkuranga.
 
Kamanda Kova amesema wanaowashikiria ni Ramadhan Ulatule (15),Mkazi wa Mandimkongo, Mkuranga, Omary Amour( 24) Mkazi Mkazi wa Mbagala Kimbangulile.
 
Kova amesema baada ya kuwabana watuhumiwa wa ujambazi walikwenda kuonyesha bunduki  15 walizopora katika kituo cha Stakishari ambazo walikuwa wamehifadhi chini ya ardhi na kuweka kinyesi juu.
 
Amesema katika Shimo walilohifadhi walikuta bunduki aina ya  Norinko ambayo wanatafuta ilipoibiwa pamoja na kukuta fedha taslimu Sh.Milioni 170 za kitanzania.
 
Aidha amesema jeshi la polisi limejizatiti katika matukio na kutaka watu waachane na biashara hiyo ya ujambazi kwa kuwa halipi.
 
Amesema fedha hizo wanazichunguza kujua zimeibwa wapi,na pikipiki mbili aina ya boxer nazo wanazishiklia na kutaka wauza pikipiki kuuzia watu ambao wanataarifa nao.
 
“Hatutafumbia macho kwa wale askari wanaojihusisha na vitendo vya kihalifu kwa kuwachukulia hatua kali ikiwa hata kama wanajihusiha na ujambazi tutawashughulikia kwani risasi haichagui kuwa huyu raia au askari” amesema Kamishina Kova.
 
Tukio la kuawawa kwa askari wanne na raia watatu katika kituo cha Stakishari,lilitokea  julai 12 majira ya saa nne.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Suleiman Kova akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kukamatwa kwa watuhumiwa wa ujambazi waliovamia kituo cha Polisi cha Stakishari, Tazara,leo jijini Dar es Salaam.
 Naibu wa Kamshina wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Simon Sirro akizungumza na waandishi wa habari juu operesheni iliyofanyika ya kuwakamata watuhumiwa wa ujambazi waliovyamia kituo cha Stakishari ,Tazara,jijini Dar es Salaam.
 Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Kamishina Suleiman Kova akionyesha bunduki zilizoporwa katika uvamizi wa uliofanywa na majambazi katika kituo stakishari,Tazara leo jijini Dar es Salaam.
  Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Kamishina Suleiman Kova akionyesha Fedha taslimu Sh.Milioni 170 zilizkutwa katika Shimo na majambazi waliovyamia kituoa stakishaari na kuua askari,leo jijiji Dar es Salaam.
 Fedha za watuhumiwa ujambazi waliovamia kituo cha Polisi cha Stakiki zikiwa katika sanduku zikionyeshwa kwa waandishi habari na wananchi leo jijini Dar es Salaam.
 Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Kamishina Suleiman Kova akionyesha picha za majambazi sugu wanaotafutwa na jeshi la polisi katika hafla ya kutuoa taarifa za kukamatwa kwa askari wa waliovamia kituo cha stakishari leo jijini Dar es salaam 
Pikipiki zilizokuwa zikitumiwa na majambazi waliovyamia Kituo cha Stakishari zikiwa mbele ya Kamisha Kova wakati akitoa taarifa kukamtwa kwao leo jijini Dar es Salaam.

Ijumaa, 10 Julai 2015

RAIS KIKWETE AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM MJINI DODOMA LEO, TANO BORA YA WAGOMBEA KUPATIKANA BAADA YA KIKAO HIKI


       
         

RAIS KIKWETE AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM MJINI DODOMA LEO, TANO BORA YA WAGOMBEA KUPATIKANA BAADA YA KIKAO HIKI

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM, Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza Kikao cha Kamati Kuu ya CCM (CC) kinachoendelea hivi sasa kwenye Ukumbi wa White House, Makao Makuu ya CCM, Mjini Dodoma. Kikao hiki kinapitia majina yote 38 ya Watangaza nia ya kugombea Urais kwa tiketi ya CCM, ambapo majina matano yatapatikana baada ya kikao hiki.Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM - Zanzibar, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein, Makamu Mwenyekiti wa CCM - Bara,...
Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete(wa pili kushoto) akiongoza kikao cha Kamati Kuu Maalum cha CCM mjini Dodoma, Kikao hicho kitachuja majina ya wagombea na kupata majina matano(5) .Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoa taarifa fupi ya wajumbe waliohudhuria kikao cha Kamati Kuu Maalum ambapo wajumbe 28 walihudhuria...

Jumanne, 7 Julai 2015

Watu 25 wauawa Zaria Nigeria



Wengi waliokuweko ni walimu na wafanyikazi wa umma.
Maafisa wa serikali Kaskazini mwa Nigeria wamesema kuwa watu 25 wameuawa katika shambulio la bomu la kujitolea mhanga katika mji wa Zaria.
Ripoti zinasema kuwa watu wengine 32 wamejeruhiwa kwenye shambulizi hilo.
Shambulio hilo lilitokea katika jengo moja la serikali ambako wafanyakazi wa serikali walikuwa wamekusanyika kusajiliwa.
 
Watu 220 wameuawa katika mashambulizi kadha yanayolaumiwa kutekelezwa na kundi la wapiganaji wa Boko Haram
Wengi waliokuweko ni walimu na wafanyikazi wa umma.
Katika kipindi cha majuma 2 yaliopita takriban watu 220 wameuawa katika mashambulizi kadha yanayolaumiwa kutekelezwa na kundi la wapiganaji wa Boko Haram.
Gavan wa jimbo la Kaduna amewaonya wenyeji kuwa waangalifu sana na kuepuka maeneo yaliyojaa watu kwani hayo ndio yanayolengwa na washambuliaji wa kujitolea mhanga.
 

Gavana Nasir El-Rufa'I amewasihi wenyeji waepuke misikiti makanisa masoko na vituo vya mabasi hadi pale hali itakapotulia.
Gavana Nasir El-Rufa'I amewasihi wenyeji waepuke misikiti makanisa masoko na vituo vya mabasi hadi pale hali itakapotulia.
Inspekta wa polisi wa Nigeria ameomba wanigeria kuwa makini na waangalifu akisema kuwa ''kwa sasa inaonekana mabomu yameundwa mengi na kwa hakika likishaundwa bomu ni vigumu sana kuzuia mashambulizi ya kujilipua kwenye umati wa watu ilikuzidisha maafa''.
Tayari hofu imetanda katika mji wa Abuja ambapo Polisi wamepiga marufuku uuzaji na uchuuzi katika barabara za katikati ya mji.

Alhamisi, 2 Julai 2015

WALIOMUUA ALBINO MWAKAJILA WA MBEYA WAHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA


Hakimu Mwakalinga siku alipohukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa mauaji ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe. Leo amehukumiwa tena kunyongwa mpaka kufa katika mauaji ya mlemavu wa ngozi Henry Mwakajila.
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Mbeya leo hii imewahukumu kunyongwa mpaka kufa watu wanne kati ya watano waliomuua Henry Mwakajila (17) ambaye ni mlemavu wa ngozi (albino).
Waliohukumiwa kunyongwa mpaka kufa ni Asangalwisye Kayuni maarufu kama Katiti au Mwakatoga na Gerard Korosso Kalonge (wakazi wa Kijiji cha Mbembati wilayani Ileje), na Leonard Msalage Mwakisole na Hakimu Mselem Mwakalinga (wakazi wa Kiwira wilayani Rungwe).
Mshtakiwa wa nne, Mawazo Philemon Figomole, ameachiliwa huru na mahakama hiyo baada ya ushahidi wa upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha pasi na shaka kwamba alihusika katika mauaji hayo.
Akisoma hukumu ya kesi hiyo ya mauaji yenye kumbukumbu Namb. KIW/IR/49/2008 na PI 5/2013, Jaji wa Mahakama Kuu Dk. Revila, amesema mahakama imejiridhisha pasi na shaka na ushahidi wa upande wa mashtaka kwamba washtakiwa hao wanne walitenda kosa hilo na hivyo wanastahili adhabu hiyo.
Hii ni kesi ya saba ya mauaji ya albino kutolewa hukumu ambapo mpaka sasa jumla ya watuhumiwa 15 wamehukumiwa kunyongwa mpaka kufa. Ililezwa mahakamani hapo kwamba, mnamo Februari 5, 2008 majira ya saa 12:00 na saa 1:00 jioni huko katika Kijiji cha Ilolo, Kata ya Kiwira, tarafa ya Ukukwe, wilayani Rungwe katika Mkoa wa Mbeya, washtakiwa hao walimteka nyara kijana Henry Mwakajila, ambaye ni mlemavu wa ngozi aliyekuwa akisoma kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Ukukwe na kisha kumuua.
Wakati wa mwenendo wa kesi, ilielezwa na mashahidi wa upande wa mashtaka kwamba mshtakiwa wa kwanza Asangalwisye Kayuni maarufu kama Katiti au Mwakatoga ambaye ni mganga wa jadi, mkazi wa Kijiji cha Mbembati, Wilaya ya Ileje, alikutwa na utumbo unaodhaniwa kuwa wa binadamu na ulipopelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ukathibitika kwamba ni utumbo wa marehemu Henry.(VICTOR)
Mshtakiwa wa pili, Gerard Korosso Kalonge wa Kijiji cha Mbembati wilayani Ileje alikutwa na vidole vinne na mifupa kumi (10) vyote vinavyodhaniwa kuwa vya binadamu na baada ya uchunguzi wa Mkemia Mkuu wa Serikali ilibainika kwamba ni viungo vya marehemu Henry Mwakajila.
Ilielezwa pia kwamba, washtakiwa Leonard Msalage Mwakisole, Mawazo Philemon Figomole na Hakimu Mselem Mwakalinga ndio waliodaiwa kumteka nyara mtoto huyo na kumuua, kisha kupeleka viungo kwa mganga wa kienyeji Asangalwisye Kayuni.
Mshtakiwa wa tano, Hakimu Mselem Mwakalinga, tayari alikwishahukumiwa kunyongwa katika kesi nyingine ya mauaji ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, John Mwankenja, ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi nyumbani kwake. Hukumu ya kesi hiyo namba 131/2012 ilitolewa Novemba 13, 2013 ambapo inaelezwa kwamba watuhumiwa walitenda kosa hilo Mei 19, 2011 katika kijiji cha Mpandapanda, Kata ya Kiwira Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya.
Ingawa watuhumiwa walikuwa wanne, lakini Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya chini ya Jaji Samwel Karua iliwahukumu kunyongwa mpaka kufa mshtakiwa wa kwanza Hakimu Mwakalinga na mshtakiwa wa pili Daudi Mwasipasa kwa maelezo kwamba walihusika moja kwa moja na mauaji hayo ya kukusudia.
Mshtakiwa namba tatu Obote Mwanyingili yeye alitiwa hatiani kutokana na kosa la kumhifadhi mtuhumiwa namba moja baada ya kutoka kufanya mauaji wakati mshtakiwa namba nne Kelvin Myovela alitiwa hatiani kutokana na kuhifadhi silaha iliyotumika katika mauaji hayo ingawa hakusika na kitendo hicho moja kwa moja, hivyo wote wawili walihukumiwa kifungo cha miaka saba jela.
Hata hivyo, Myovela tayari alikwishahukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa kukutwa na silaha kinyume cha sheria.
Inadaiwa kwamba, chanzo cha mauaji hayo ya John Mwankenja, ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Rungwe, kilitokana na kiongozi huyo kufahamu kwamba hao ndio waliomuua mlemavu wa ngozi Henry Mwakajila, hivyo aliuawa ili kupoteza ushahidi