Jumatano, 29 Julai 2015

Job Ndungai amshushia kipigo mgombea mwenza.

Mtia nia wa Jimbo la Kongwa, Dk. Joseph Chilongani akiwa amelazwa hospitali mjini Kongwa
 Mtia nia wa Jimbo la Kongwa, Dk. Joseph Chilongani akiwa amelazwa hospitali mjini Kongwa


NAIBU Spika na Mbunge wa Jimbo la Kongwa Job Ndugai amemshushia kipigo mgombea mwenzake Dk.Joseph Chilongani na kusababishwa kuzirai na kukimbizwa katika hospitali ya Wilaya ya Kongwa. Anaandika Dany Tibason, Kongwa, Dodoma … (endelea).
Ndugai alimpiga kwa fimbo Dk. Chilongani kutokana na kitendo chake cha kutumia simu yake ya mkononi kurekodi matukio ya ubishani baina yao na Saimon Ngatunga.
Akizungumza na gazeti hili, mdogo wa mgombea huyo Michael Chilongani alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 10 jioni katika Kata ya Ugogoni mjini Kongwa wakati wakiwa kwenye kampeni ya kujinadi kwa wanachama.
Amesema ndugu yake huyo amepigwa fimbo kichwani na tumboni na kusababisha kupoteza fahamu kwa zaidi ya saa mbili ambapo alikimbizwa kituo cha polisi kwa ajili ya kupatiwa fomu namba tatu na kisha kupelekwa hospitali.
Ndugai alimshushia kipigo mwenzake baada baada ya mgombea aliyetangulia kudai kwamba iwapo Chama kitampa ridhaa ya kuwania nafasi ya ubunge hatahakikisha anapambana ubadhirifu wa fedha katika halmashauri.
‘Baada ya fahamu kumrudia majira ya saa moja na nusu usiku, kaka alidai anasikia maumivu makali kwenye paji la uso pamoja na kichwani huku akipata shida kuzungumza,’ amesema.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo waliliambia gazeti hili kuwa kabla ya Dk. Chilongani kujeruhiwa kwa fimbo na mgombea mwenzake alitaka kumpiga fimbo hiyo mgombea mwingine aliyejinadi kuwa atakomesha ubadhirifu katika halmashauri ambapo kamati ya ulinzi iliwahi kumzuia.
Naye Kaimu Katibu wa CCM wilaya ya Kongwa Peter Minja amesema kila mgombea ambaye anamalalamiko ayapeleke katika vikao husika.
Kuhusu vurugu za ndugai kumpiga mwenzake amesema mpaka sasa hawajapokea malalamiko yoyote kwa utaratibu unaotakiwa na badala yake wamekuwa wakipokea malalamiko ya maneno.
Alipotafuwa Mkuu wa polisi Mkoa wa Dodoma David Misime alipotakiwa kuzungumzia suala hilo kama amepokea taarifa za Ndugai kumpiga mwenzake amesema hana taarifa .
Amesema hayupo ofisini na akiwa ofisini na kupata taarifa ataweza kuviarifu vyombo vya habari.
NAIBU Spika na Mbunge wa Jimbo la Kongwa Job Ndugai amemshushia kipigo mgombea mwenzake Dk.Joseph Chilongani na kusababishwa kuzirai na kukimbizwa katika hospitali ya Wilaya ya Kongwa.
Ndugai alimpiga kwa fimbo Dk.Chilongani kutokana na kitendo chake cha kutumia simu yake ya mkononi kurekodi matukio ya ubishani baina yao na Saimon Ngatunga.
Akizungumza na gazeti hili, mdogo wa mgombea huyo Michael Chilongani alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 10 jioni katika Kata ya Ugogoni mjini Kongwa wakati wakiwa kwenye kampeni ya kujinadi kwa wanachama.
Amesema ndugu yake huyo amepigwa fimbo kichwani na tumboni na kusababisha kupoteza fahamu kwa zaidi ya saa mbili ambapo alikimbizwa kituo cha polisi kwa ajili ya kupatiwa fomu namba tatu na kisha kupelekwa hospitali.
Ndugai alimshushia kipigo mwenzake baada baada ya mgombea aliyetangulia kudai kwamba iwapo Chama kitampa ridhaa ya kuwania nafasi ya ubunge hatahakikisha anapambana ubadhirifu wa fedha katika halmashauri.
‘Baada ya fahamu kumrudia majira ya saa moja na nusu usiku, kaka alidai anasikia maumivu makali kwenye paji la uso pamoja na kichwani huku akipata shida kuzungumza,’ amesema.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo waliliambia gazeti hili kuwa kabla ya Dk. Chilongani kujeruhiwa kwa fimbo na mgombea mwenzake alitaka kumpiga fimbo hiyo mgombea mwingine aliyejinadi kuwa atakomesha ubadhirifu katika halmashauri ambapo kamati ya ulinzi iliwahi kumzuia.
Naye Kaimu Katibu wa CCM wilaya ya Kongwa Peter Minja amesema kila mgombea ambaye anamalalamiko ayapeleke katika vikao husika.
Kuhusu vurugu za ndugai kumpiga mwenzake amesema mpaka sasa hawajapokea malalamiko yoyote kwa utaratibu unaotakiwa na badala yake wamekuwa wakipokea malalamiko ya maneno.
Alipotafuwa Mkuu wa polisi Mkoa wa Dodoma David Misime alipotakiwa kuzungumzia suala hilo kama amepokea taarifa za Ndugai kumpiga mwenzake amesema hana taarifa .
Amesema hayupo ofisini na akiwa ofisini na kupata taarifa ataweza kuviarifu vyombo vya habari.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni