Jumatano, 13 Desemba 2017

RAIS MAGUFULI ATOA ONYO KALI BENKI KUU YA TANZANIA BOT

Rais Dkt. John Pombe Magufuli amewapa onyo la mwisho Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na kuwataka wawe wasimamizi wazuri wa fedha za nchi na kusema kama hawatajirekebisha basi wasijekumlaumu siku za usoni.

Magufuli amesema hayo leo alipokuwa akizindua tawi moja la Benki mjini Dodoma na kuzitaka benki zote pamoja na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuangalia suala la matumizi ya fedha za kigeni ndani ya nchi kwani jambo hilo linazidi kuuwa uchumi wa nchi.

"Haiwezekani nchi ikawa na 'curency' mbili,  tatu au zaidi zinazotumika zinaharibu uchumi, haiwezekani mtu ukiwa na dollar unakwenda kununua bidhaa dukani, ukiwa na pounds unakwenda kununua chochote nchini huu si utaratibu wa uchumi. Na hili nikuombe Waziri,  BoT na mabenki yote mlisimamie hili kikamilifu, na baya zaidi haya yamekuwa yakifanywa na BoT. Gavana upo hapa mnapotangaza tenda zenu hata za wafagiaji mnawalipa kwa Dollar .

"Sasa haiwezekani nyinyi BoT ambao mnasimamia fedha nyinyi hao hao mnakuwa wabaya wa kudhibiti fedha za nchi hili lazima muende nalo na mbadilishe haraka. 
"Msije kuwa chanzo cha kuharibu uchumi wa nchi yetu. Najua mnanielewa nililizungumza jambo hili mara ya kwanza nimelirudia leo mara ya mwisho litakalotokea msije kunilaumu" alisisitiza Rais Magufuli

Mbali na hilo Rais Magufuli amehitaji kuwe na uangalizi mzuri kwenye 'Bureau de Change' na kuwa na utaratibu ambao unaeleweka.

Advertisement
==

Jumatano, 30 Agosti 2017

Muda wa mwisho wa kuwasilisha maombi ya mikopo sasa ni Septemba 11 badala ya Septemba 4

Wednesday, August 30, 2017

Muda wa mwisho wa kuwasilisha maombi ya mikopo sasa ni Septemba 11 badala ya Septemba 4

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imeongeza muda wa wanafunzi kuwasilisha maombi ya mikopo. Hatua hiyo imeelezwa inalenga kutoa nafasi kwa wanafunzi walioshindwa kufuata masharti kuyakamilisha. Mkurugenzi Mkuu wa bodi hiyo, Abdul-Razaq Badru amesema muda huo umeongezwa hadi Septemba 11 badala ya Septemba 4. "Tumesogeza mbele kwa siku saba zaidi ili walioshindwa kufuata...
Read More

Alhamisi, 22 Desemba 2016

Majambazi Wawili Wauawa Jijini Mbeya Katika Mapambano Makali Kati Yao Na Jeshi La Polisi

Wednesday, December 21, 2016

Majambazi Wawili Wauawa Jijini Mbeya Katika Mapambano Makali Kati Yao Na Jeshi La Polisi

Askari wa Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya wamefanikiwa kuzuia tukio la ujambazi katika mapambano ya kurushiana risasi na watu waliosadikiwa kuwa ni majambazi na kuua wawili kati yao.

Taarifa iliyotolewa leo na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Dhahiri Kidavashari imesema kuwa mnamo tarehe 19.12.2016 majira ya saa 1:45 jioni katika Kijiji cha Busisya, Wilaya ya Rungwe, Askari Polisi walipata taarifa za siri za kuwepo kwa majambazi wenye silaha ambao walikuwa na lengo la kufanya uvamizi katika Duka la Mfanyabiashara wa soda na bia za jumla ambaye pia ni wakala wa kutuma na kupokea pesa kwa njia ya mtandao.

Askari hao walianza kuwafuatilia majambazi hao na muda wa saa 1:45 jioni askari walikutana na majambazi hao wakiwa wamepakiana katika pikipiki ambapo baada ya majambazi hao kugundua kuwa wanafuatiliwa na askari walianza kuwarushia risasi askari na ndipo yalitokea majibizano ya risasi kati ya askari na majambazi hao.

Askari walifanikiwa kuwapiga risasi majambazi wawili ambao walifariki papo hapo na mmoja wao aliweza kutupa silaha aliyokuwa akiitumia na kukimbia.

Aidha katika tukio hilo silaha bunduki tatu pamoja na risasi tisa ziliweza kupatikana zilizokuwa zinatumiwa na majambazi hayo. Silaha hizo ni Mark IV yenye namba 38482 na risasi mbili, Short Gun Greener yenye namba G.73878 na risasi 01 na Gobole lililotengenezwa kienyeji ambalo halina namba na risasi 06.

Pia baada ya kupekuliwa majambazi hao walikutwa na vitu vingine ambavyo ni Rungu moja, Praizi moja, Bisibisi moja, mafuta ya cherehani, koti la ngozi rangi ya brown pamoja na begi dogo rangi nyeusi ambalo lilitumika kuhifadhi vitu hivyo.

Miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Serikali Makandana Wilaya ya Rungwe kwa uchunguzi wa kitabibu na bado haijatambulika. Msako unaendelea. Katika tukio hilo hakuna mali iliyoporwa wala askari kupata madhara. Jitihada za kumtafuta jambazi aliyekimbia zinaendelea, Upelelezi unaendelea.

Rais wa Gambia: Hakuna wa kunitoa Madarakani, labda Mungu Pekee

Rais wa Gambia: Hakuna wa kunitoa Madarakani, labda Mungu Pekee

Rais wa Gambia Yahya Jammeh amesema kuwa atakataa jaribio lolote la viongozi wa eneo la magharibi mwa Afrika la kumlazimisha kuondoka madarakani licha ya kushindwa katika uchaguzi na mpinzani wake, Adama Barrow.

Akihutubia Wanachama wa Muungano nchini humo Bw. Jammeh amesema: ”Waje wajaribu kuniondoa wanasubiri nini? mimi ni mtu mpenda amani lakini haimaanishi kwamba sitalitetea taifa langu, kwa ujasiri na uzalendo na kuibuka mshindi”.

“Mimi sio muasi, haki yangu haiwezi kuvurugwa. Hii ni nafasi yangu, hakuna mtu anayeweza kuniondoa labda Mungu,” amesema.

Amesema kuwa alikataa wito wa Muungano wa Viongozi wa Mataifa ya Magharibi ECOWAS akiwemo Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria na Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia kuondoka nchini Gambia.

“’Wao ni kina nani wa kuniambia mimi niondoke nchini mwangu,” amesema na kuwashutumu viongozi hao kwa kuingilia mambo ya ndani ya Gambia.

ECOWAS tayari imesema kuwa inamtambua Bw. Barrow kama Rais wa taifa hilo na kwamba litachukua hatua zozote kuhakikisha kuwa matokeo ya uchaguzi yanaheshimiwa.

Viongozi wa eneo hilo watahudhuria kuapishwa kwa Bw. Barrow mnamo mwezi Januari 18 kulingana na taarifa ya Ecowas.

Rais Jammeh awali alikuwa amekubali matokeo ya uchaguzi huo mnamo Desemba 1, 2016 lakini baadaye akaitisha uchaguzi mpya utakaoandaliwa na tume ya uchaguzi inayomcha Mungu kwa madai kuwa matokeo hayo uchaguzi yaligubikwa na dosari.




Ijumaa, 7 Oktoba 2016

MAMBO NI MAZURI KWELI KWELI NGOMA ZINAENDELEA KICHUANA VIBAYA SANA





MPAMBANO BADO NI MKALI SANA WA NGOMA HIZI ZA KINYAKYUSA
USIKAE MBALI TUTAENDELEA KUKUJUZA KINACHOJILI.

TAMASHA LA NGOMA ZA ASILI LILILOANDALIWA NA MHE. TULIA A. MWANSASU NAIBU SPIKA WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, LINAENDELEA KATIKA VIWANJA VYA TANDALE TUKUYU MJINI

 HAPA NDO UWANJA WA MPIRA TANDALE MASINDANO YA NGOMA YANAENDELEA



 MEZA KUU WAKIJIANDAA KUMPOKEA BAROZI WA KENYA TANZANIA
TULIA AKIMPOKEA BAROZI WA KENYA 


 WAANDISHI WA HABARI WAKIWA MAKINI KUCHUKUA MATUKIO 




MASHINDANO HAYA YA NGOMA ZA ASILI YA WANYAKYUSA NI MWENDELEZO WA KUZITANGA NGOMA HIZI KITAIFA NA KIMATAIFA ILI IWE NI AJILA KWA VIJANA NA WASANII WA NGOMA ZA ASILI. 

TUTAENDELEA KUWAJUZA KINACHOENDELEA UWANJANI HAPA USICHEZE MBALI


Alhamisi, 29 Septemba 2016

MASHINDANO YA NGOMA ZA ASILI ZA KINYAKYUSA YALIYOANDALIWA NA MHE. ATUPELE MWAKIBETE MBUNGE WA BUSOKELO YALIFANYIKA KANDETE NA ITETE.



 Viongozi wakiwa wanaburudika na Ngoma za Asili
 

Ngoma zikiendelea na Mashindano.






 Viongozi wa Ngoma wakiwa Mbele ya Mgeni rasmi 
Mhe.Tulia A.Mwansasu Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Mashindano ya Ngoma za Asili ya wanyakyusa yaliyofanyika Itete wilayani Busokelo yalifanyika pia Wilayani Rungwe na Kyela.

Lengo la mashindano hayo ni kuutangaza Utamaduni wa Ngoma za asili ya wanyakyusa kwa ngazi ya kitaifa na kimataifa.

Wazo hilo alilitoa Mhe. Tulia A. Mwansasu Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwashilikisha wabunge watatu wanaounganisha jamii nzima ya wanyakyusa ya Rungwe,Busokelo na Kyela Mhe. Sauli Amoni Mbunge Jimbo la Rungwe, Mhe. Atupele Mwakibete Mbunge Jimbo la Busokelo na Mhe. Harison Mwakyembe Mbunge wa Jimbo la Kyela.

Kwa pamoja wakafikia makubaliano ya kila Mmoja akanzishe mashindano ya Ngoma Hizo kuanzia Ngazi ya Kata kwa kila kata kutoa Ngoma Moja kwenda ngazi ya Wilaya na kila wilaya kutoa ngoma Moja kwa mashindano ya wilaya au majimbo matatu yani Rungwe, Busokelo na Kyela.

Mashindano hayo ya Majimbo matatu yatafanyika kuanzia tarehe 7 - 8/10/2016.

Mashindano kwa ngazi ya Kata na Wilaya au jimbo yanaandaliwa na wabunge wa majimbo na mashindano ya wilaya tatu au majimbo matatu znaandaliwa na Mhe. Tulia A. Mwansasu Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mashindano hayo yatafanyika katika mji wa Tukuyu katika viwanja vya Tandale. 

Na Rungwe Yetu.