Jumatano, 11 Machi 2015

TUKIO KATIKA PICHA NA TAARIFA YA AWALI KUTOKA JESHI LA POLISI MKOA WA IRINGA KUTOKANA NA AJALI YA BASI LA ABIRIA NA LORI ILIYOTOKEA MAPEMA LEO .

 Mashuhuda wa ajali hiyo wakijaribu kuokoa mizigo


 kikosi cha uokoaji wakiwa katika harakati za kulitoa kontena juu ya basi na kutoa miili ya marehemu
 Winchi zikilitoa kontena juu ya basi
 Muonekano wa basi hilo Baada ya kulitoa kontena juu 



 Taarifa za awali kutoka jeshi la polisi mkoani Iringa zinaeleza kuwa basi la kampuni Majinja lenye usajili wa namba T438 CDE lililolaliwa na Lori lilikuwa limebeba jumla ya watu 49, idadi hiyo ni pamoja na dereva na kondakta wa basi hilo.wengi wa watu hao wamefariki dunia idadi ya majeruhi haijajulikana bado. 

 Taarifa hizo zinaeleza kuwa kwenye mizigo mingi ya abiria waliokuwa kwenye basi hilo kumepatikana madaftari mengi ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salaam hivyo jeshi hilo linaendelea kufanya mawasoliano ma wamiliki wa gari hilo ili kujua kama lilikuwa limekodishwa kubeba wanafunzi wa chuo hicho ama ni mchanganyiko wa kawaida wa abiria.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni