Jumatano, 11 Machi 2015

Ajali imetokea changalawe Mafinga



Breaking News:  kwa Taarifa tulizopokea muda huu na ambazo hazijathibitishwa kuwa Basi la Majinja Limepata ajali eneo la Mafinga likitokea Mbeya na inahofiwa watu wengi kupoteza maisha. chanzo mpaka sasa inasemekana ni Lori lilikuwa linakwepa mashimo ,na ndipo likagongana uso kwa uso na Basi hilo Taarifa kamili na Tukio katika Picha zitafuata mara baada ya kupata uhakika kamili endelea kufuatilia hapa, Tayari Kikosi kazi cha Blogs ya rungwe yetu kipo eneo la tukio.

Hawa ni Baadhi ya Merehemu waliokwama katika basi wanaohofiwa kufa katika ajali hiyo

 Nusu ya basi likiwa limepondwa na kontena


Watu wapatao 50 wanahofiwa kufa papo hapo baada ya basi hilo la Majinja Express kugongana na lori na kuangukiwa na kontena

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni