Jumatatu, 2 Machi 2015

MPYAA MSANII WA BONGO MOVIE MWANADADA CHUCHU AZIRAI NDANI YA JENEZA WAKATI WA KUSHUTI MOVIE


HII ni kali ya mwaka! Staa wa sinema za Bongo, Chuchu Hans amejikuta akizirai ndani ya jeneza wakati akiigiza sini ya kifo kwenye filamu, Amani limeinyaka.
Staa wa sinema za Bongo, Chuchu Hans akiwa kwenye jeneza.
Chuchu alikumbwa na hali hiyo hivi karibuni akiwa ‘lokesheni’ ya kuigizia filamu hiyo maeneo ya Mbezi ya Kimara jijini Dar es Salaam ambapo sanjari na yeye, msanii mwingine aliyecheza nafasi ya mwanakwaya naye alipoteza fahamu wakati kipande hicho kikirekodiwa.
TATIZO UHALISIA, WASIWASI
Chanzo kimoja kutoka ndani ya kundi la wasanii waliokuwa wakiigiza filamu kinasema kuwa, Chuchu alikumbwa na hali hiyo kutokana na wasiwasi na ujasiri wa kuuvaa uhusika.
“Awali, Chuchu alionesha wasiwasi wa kuigiza kipande hicho cha kumwonesha yeye yumo ndani ya jeneza akiwa amefariki dunia kwa ugonjwa kama wa kichaa kilichotokana na msongo wa mawazo baada ya kubakwa.
“Mbaya zaidi, mwongozaji naye alisema ni lazima akiwa amelala ndani ya jeneza awekewe pamba za kuziba matundu ya pua kama maiti wanavyowekewa,” kilisema chanzo.
...Waombolezaji wakilia kwa uchungu.
ILIKUWA WAKATI AKIAGWA
Chanzo kikazidi kudai kwamba, taharuki yote hiyo ilitokea pale, ‘mwili’ wa Chuchu ukiagwa kwenye Kanisa la Sabato, Mbezi, Dar ambapo waombolezaji walipokuwa wakipita, binti yake, Farha (9) aliangua kilio kilichomfanya Chuchu ajikute akikata pumzi ghafla!
AMALIZA SINI, ASHINDWA KUAMKA
Ikaelezwa kwamba, ilikuwa wakati kipande hicho kimeisha huku binti yake akiendelea kulia kwa kumwona mama yake ndani ya jeneza, Chuchu hakuamka ili kuendelea na vipande vingine hali iliyowafanya watu wazima kumkagua na kugundua alizirai.
“Watu walianza kupagawa, wengine walijua ameshapoteza maisha. Lakini Mungu mkubwa Chuchu akazinduka na kumkuta mwanaye bado akilia kwa nguvu. Ilibidi wasanii wengine waingilie kati kumtuliza,” kilisema chanzo.
Waombolezaji wakiwa na simanzi.
MWINGINE AITIWA MCHUNGAJI
Wakati Chuchu ‘akifufuka’, yule msanii aliyeigiza nafasi ya mwanakwaya yeye alikuwa bado chini amelala chali akiwa hajitambui kwa kile kilichokuwa kikiendelea.“Yule mwenzake ilibidi aitwe mchungaji wa kanisa hilo ambaye alikuwa jirani kwa ajili ya kumwombea japo mchungaji wa filamu hiyo alikuwa ni msanii Jimy Mafufu,” kilisema chanzo.
MASWALI ENEO LA TUKIO
Baadhi ya wasanii walianza kujiuliza nini kilisababisha hali ile kwani ilionekana kama kuna roho chafu aliyetaka kufanya mauaji ya makusudi.
“Wengine waliuliza kama kuna mtu ana vitu kama hirizi au chanjo ya mambo ya kishirikina, ikaonekana hakuna. Lakini maswali yalikuwa mengi sana,” kilisema chanzo.

Jeneza likiandaliwa kwa ajili ya mazishi.
CHUCHU AONGEA NA AMANI
Baada ya kuinasa taarifa hiyo, Amani lilimsaka Chuchu kwa njia ya simu yake ya mkononi na kumuuliza ambapo alikiri kutokea kwa tukio hilo.
Huyu hapa:  “Yaani siwezi kueleza juu ya ile filamu maana ilikuwa ni hatari tupu na sijui hata mama yangu akiiona itakuaje kwa kweli.
“Lakini kwenye ile sini yangu ndiyo ilikuwa ikihitaji hivyo, nilale kama maiti kweli na huwezi amini lilichimbwa hadi kaburi la ukweli. Mimi nilizimia si chini ya  mara moja. Pumzi yangu ilikata hasa nilipomsikia mwanangu akilia.”
CHUCHU ANAWEZA ASIWE SAWA KISAIKOLOJIA
Kwa mujibu wa maswali ya kisaikolojia kwa wasanii wa maigizo, baada ya msanii kuigiza filamu inayohusu ukatili wowote, kumwaga damu, mapenzi ya kupitiliza, kifo au jambo lolote ambalo ni chungu kwa ubinadamu ni lazima aombewe na viongozi wa dini ili kuifukuza roho hiyo ya kuigizia.
Wanasaikolojia wanasema kuwa, msanii akiigiza nafasi kama hizo na kujiacha hivihihivi kuna hatari baada ya muda kuambukizwa na uigizaji huo ikawa ndiyo maisha yake ya kila siku. Ndiyo maana baadhi ya wasanii wa filamu duniani kote wanaishi maisha ya sawasawa na wanavyocheza filamu. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni