Jumanne, 2 Desemba 2014

WAFANYAKAZI WA BENKI YA NMB MBEYA MJINI WASHEREHEKEA SIKU YA FAMILIA.

Meneja wa Kanda, Lecrisia Makiriye, alisema benki inathamini mchango wa watumishi pamoja na familia zao ndiyo maana hutenga siku moja kwa ajili ya kukutana.

Baadhi ya wafanayakazi wa benki ya NMB Mbeya wakifanya mazoezi siku hiyo ya Familia ya NMB


Meneja wa Kanda, Lecrisia Makiriye, akiwa na watumishi wenzake wakibadilishana mawazo katika siku hiyo 

Baadhi ya watoto wa wafanyakazi wa NMB wakiwa na wazazi wao katika siku hiyo ya familia ya NMB


Mazoezi ya viungo yanaendelea

Watoto wakicheza michezo mbalimbali katika uwanja wa Ifisi Mbeya



Mpira wa miguu ulikuwepo pia


Makirikiri ya Mbeya nao wakiendelea kuwaburudisha wanafamilia wa NMB


Nifuraha kwa watoto na wazazi pia

Meneja wa Kanda, Lecrisia Makiriye, akitoa zawadi kwa watoto walioshiriki mashindano mbalimbali katika siku hiyo ya wanafamilia ya NMB

Watoto wakiwashukuru wazazi wao kwa zawadi na kujumuika pamoja katika sherehe hiyo kwani kumewafanya wafahamiane na watoto wenzao na kupata marafiki wapya



Mashindano ya kuvuta kamba



Watoto wakikabidhiwa zawadi ya kuku mara baada ya kushinda kuwakamata kuku hao


Picha ya pamoja ya wanafamilia wa NMB Mbeya

WAFANYAKAZI wa Benki ya NMB Mbeya mjini wameungana na familia zao kusherehekea siku ya Familia iliyofanyika katika viwanja vya Ukumbi wa Mikutano wa Ifisi.
Akizungumza katika sherehe hizo Meneja wa Kanda, Lecrisia Makiriye, alisema benki inathamini mchango wa watumishi pamoja na familia zao ndiyo maana hutenga siku moja kwa ajili ya kukutana.
Aidha alitoa wito kwa wazazi na walezi kuwalea watoto wao katika maadili mema na mazuri kwa kuwaepusha kujiingiza katika vitendo viovu ili siku moja waje kuwa watumishi katika fani mbali mbali kwa manufaa ya taifa.
Meneja huyo aliwaambia wanafamilia wa NMB kuwa Benki hiyo imekuwa kubwa kiasi kwamba shughuli zake zimeongezeka na kufikia kuwa na matawi mengi zaidi kuliko benki yoyote nchini pamoja na ATM zaidi ya 400 nchi nzima hivyo wanapaswa kushirikiana.
Katika Sherehe hizo Wanafamilia wa NMB walishiriki mazoezi ya viungo pamoja na michezo mbali mbali ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa wavu, kuvuta kamba, kukimbia kwenye magunia na kukimbiza kuku pamoja na chemsa bongo kwa watoto.
Mwisho.
by  Richard mchina

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni