Ijumaa, 12 Desemba 2014

MAHAFALI YA 49 YA CHUO CHA ELIMU YA BIASHARA(CBE) KAMPASI YA MBEYA YAFANA.



Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Musa Uledi akitoa tamko la kuwatunuku vyeti vya Astashahada katika fani za ununuzi na ugavi, uhasibu na uendeshaji wa biashara Wahitimu 37 katika mahafali ya 49 ya Chuo cha Elimu ya biashara (CBE) Kampasi ya Mbeya yaliyofanyika katika viwanya vya Mbeya Hotel. 

Mkuu wa Chuo cha elimu ya Biashara Kampasi ya Mbeya, Dionise Lwanga akitoa neno la Shukrani kwa mgeni rasmi baada ya kumaliza kuwatunuku wahitimu katika mahafali ya 49 ya Chuo hicho.


Makamu mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara(CBE), Taaluma, utafiti na Ushauri Dk.Mbise akizungumza jambo katika Mahafali ya 49 ya Chuo hicho Kampasi ya Mbeya.


Afisa Taaluma wa Chuo cha Elimu ya Biashara Kampasi ya Mbeya, Thotnant Kayombo akisoma majina ya Wahitimu wa fani mbali mbali katika Mahafali ya 49 ya Chuo hicho yaliyofanyika katika viwanja vya Hotel ya Mbeya.


Afisa Uhusiano wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Leonidas Tibanga ambaye alikuwa mshehereshaji katika mahafali ya 49 ya Chuo hicho Kampasi ya Mbeya  akiendelea na shughuli zake.


Wahitimu wakivaa kofia zao baada ya kutunukiwa vyeti na mgeni rasmi katika Mahafali ya 49 ya CBE


Baadhi ya Wahitimu wakionesha nyuso za furaha baada ya kutunukiwa vyeti


Mwanafunzi aliyefanya vizuri katika masomo yake, Eliesia Mwalwibaakipokea zawadi kutoka kwa mgeni rasmi.


Baadhi ya Wahadhiri wakifuatilia kwa makini shughuli za mahafali


Kikundi cha burudani cha Kihumbe kikionesha makeke yake kwa wahitimu wazazi na wageni waalikwa katika mahafali


Picha ya Pamoja kati ya Wahadhiri na mgeni rasmi


Picha ya pamoja kati ya Wanafunzi waliofanya vizuri na meza kuu


Picha ya pamoja kati ya wahitimu na meza kuu.                           

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni