Jumatatu, 15 Desemba 2014

Magari ya Movie ya James Bond yaibiwa.


2015-land-rover-range-rover-sport-svr-front-end-in-motion
Dunia haishi vituko ambavyo hutokea kila siku na vinatokea kwa style za tofauti huku kila kinachotokea baada ya kingine kikikuacha mdomo wazi huku ukiamini kuwa hakuna kinachoweza kutokea zaidi ya hicho .
Nchini Ujerumani watu wasiojulikana wameiba magari tofauti ya kifahari yaliyokuwa yamepangwa kutumika kwenye Movie Mpya ya James Bond .
Cover la Movie ya James Bond ya The Spectre itakayotoka mwaka 2015.
Cover la Movie ya James Bond ya The Spectre itakayotoka mwaka 2015.
Magari hayo ambayo thamani yake halisi ni paundi laki sita 630,00/=  ambayo kwa fedha za Kitanzania ni zaidi ya bilioni 1 yalikuwa yatumike kwenye Toleo jipya katika mfululizo wa Movie za James Bond katika Movie itakayoitwa The Spectre.
Kampuni ya Land Rover ambayo magari hayo yametengenezwa chini yake imethibitisha kutokea kwa wizi huo na imliacha suala hilo kwa uongozi wa polisi uweze kulishughulikia .
james-bond-spectre-960x960
Kinara wa filamu hizo kwa sasa Daniel Craig ameizungumzia filamu hiyo Mpya ya The Spectre itakayotoka mwakani Tarehe 6 Novemba ambapo amesema kuwa itakuwa nzuri pengine kuliko hata ile ya mwisho ya The Skyfall ambayo iliingiza zaidi ya dola bilioni $1.1 katika mauzo yake .
Muigizaji huyo hakuzungumzia wizi wa magari hayo labda kwa kuwa tayari suala hilo liko chini ya vyombo husika .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni