Jumatatu, 24 Novemba 2014

Wavuvi 50 wauawa na Boko Haram

Taarifa kutoka Kaskazini Mashariki mwa Nigeria zinasema kuwa wanamgambo wa Boko Haram wamefanya shambulizi lengine kubwa sana na kuwaua takriban wafanya biashara 50 wa kuuza Samaki katika ufuo wa ziwa Chad.
Shambulio hilo lilifanyika Alhamisi lakini kutokana na matatizo ya kimitambo, taarifa za mauaji hayo hazikuweza kutolewa punde yalipofanyika.
Siku moja kabla ya mauaji hayo, zaidi ya watu arobaini waliuwa na wanamgambo hao, katika shambulizi lililofanya peupe mchana katika jimbo la Borno.
Wafanyabiashara hao, walikuwa njiani kununua Samaki waliposhambuliwa na wapiganaji wa Boko Haram.
Boko Haram waliziba barabara karibu na kijiji cha Doron Baga na kulingana na kiongozi mkuu wa shirika la wafanyakazi hao wakawachinja wengi wa waathiriwa wengine wakifungwa kamba na kuzamishwa majini katika ziwa Chad


Maelfu ya watu wameachwa bila makao kufuatia harakati za kundi hilo Kaskazini Mashariki mwa Nigeria
Nia ya shambulizi lao haikujulikana mara moja.Eneo lililoshambuliwa linapaswa kuwa na kikosi cha wanajeshi kinachoshika doria, lakini kikosi cha wanajeshi hao kutoka Nigeria , Chad na Niger hakijaweza kudhibiti hali katika eneo lenyewe kama ilivyotarajiwa kwani wameshindwa kulikomesha kundi la Boko Haram kufanya mashambulizi ya mara kwa mara.
Hili lilikuwa shambulizi la pili kubwa kufanyika katika jimbo la Borno wiki jana na kwa jumla takriban watu 100 waliuawa.
Mnamo siku ya Jumatano, wapiganaji hao walivamia soko moja katika eneo la Aazara Kuya. Watu 45 walikamatwa huku wakifungwa mikono na kukatwa koo zao.
Shambulizi hili inaarifiwa lililengwa kuadhibu jamii baada ya wanamgambo wanne kutambulishwa kwa wanajeshi na kuuawa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni