Jumatatu, 24 Novemba 2014

Upinzani Nigeria walaani uvamizi

Uchaguzi utafanyika mwezi Februari nchini Nigeria


  Chama cha upinzani nchini Nigeria, kimelaani uvamizi uliofanywa na maafisa wa usalama dhidi ya ofisi zake mjini Lagos mwishoni mwa wiki.
"Tunataka uchunguzi huru ufanywekubaini sababu zilizopelekea maafisa waliokuwa wamejihami kuvamia ofisi zetu, '' alisema naibu mwenyekiti wa chama cha upinzani cha (APC) Lawal Shuaibu t
Chama hicho kilisema ,komputa zake pamoja na nyaraka nyinginezo ziliporwa wakati wa msako huo.

Wakuu wa usalama wanasema wanachunguza madai ya chama hicho kutengeza kadi bandia za wapiga kura kabla ya uchaguzi kufanyika mwezi Februari.

Maafisa wa usalama walidai kuwa chama hicho kilikuwa kinatengeza kadi bandia kwa lengo la kuvamia mtandao wa tume ya uchaguzi kwa lengo la kubadilisha data ya tume hiyo.
Kwa sasa maafisa wa usalama wameweka vifaa vya udukuzi kwa ofisi hio baada ya kuhakikisha kuwa baadhi ya shughuli zinazoendelea katika jengo hilo, zinakwenda kinyume na sheria.

Chama hicho kimesema kuwa maafisa wa usalama walitwaa nyaraka, tarakilishi na vifaa vingine vya kielektroniki.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni