Jumatatu, 22 Juni 2015

JOHN MWAMBIGIJA A.K.A (MZEE WA UPAKO) ATIKISA MJI WA TUKUYU WAKATI AKIRUDISHA FOMU YA UBUNGE, MAELFU YA WATU WAJITOKEZA NA MAGARI, PIKIPIKI WASABABISHA BARABARA YA K/ROAD KUFUNGWA KWA MUDA.

Hizi ni Ofisi za Chadema Jimbo la Rungwe Magharibi Tukuyu Mjini.


Huyu Ndio John D. Mwambigija Mtiania Ubunge jimbo la Rungwe Magharibi kwa 
Tiketi ya Chadema.

Jinsi wananchi wa Rungwe walivyojitokeza kwa wingi kumuunga mkono Mtiania John Mwambigija wakati anarudisha Fomu.
 John Mwambigija Katikakati akiongozana na wananchi kuelekea katika Ofisi za Jimbo la Rungwe Magharibi.

 Mwenyekiti wa jimbo la Rungwe Magharibi, Juma Kibo akipokea fomu kwa mtiania John Mwambigija.


                                         Wananchi wakiwa Nje wakimsubiri John Mwambigija.

 Red Briged wakihakikisha Ulinzi na usalama Unazingatiwa.



                Mwenyekiti wa Jimbo Juma kibo akiwashukuru wananchi waliomsindikiza 
                            John  Mwambigija wakati wa kurudisha Fomu.
  
Mtiania John Mwambigija akizungumza neno la shukrani kwa wananchi waliomsindikiza kurudisha fomu.


............................................................................



IMEELEZWA kuwa umati mkubwa uliofurika kumsindikiza kurudisha fomu ya ubunge wa jimbo la Rungwe Magharibi John Mwambigija (CHADEMA) kutairahisishia kamati tendaji kufanya maamuzi sahihi katika kumpata mgombea anayekubarika.
kauli hiyo imetolewa na mwenyekiti wa jimbo hilo Juma kibo wakati akiwashukuru maelfu ya wananchi waliojitokeza kumsindikiza mtia nia huyo wakiwa na magari zaidi ya hamsini na pikipiki mia mbili na kupelekea makada wa CCM kushikwa na mshangao.
alisema zaidi ya watia nia 24 waliochukua fomu ni mtia nia mmoja pekee ndiyo aliyerejesha fomu saa tisa alasiri ya tarehe 22/06/2015,na kuwataka wananchi kufanya hivyo kwa watia nia wengine ili kumpata mgombea atakayepeperusha bendera katika uchaguzi mkuu wa Oktober mwaka huu.
John Mwambigija (Mzee wa upako) mbali na kuwapongeza wananchi na makada wa chama hicho waliojitokeza kwa wingi kumsindikiza kurudisha fomu,amesema pindi chama kitakapompitisha na kutwaa ubunge atahakikisha anaziondoa changamoto zilizopo na kuleta usawa kwa wana Rungwe.
Alisema wilaya ya Rungwe inavyanzo vingi vya mapato ikiwemo viwanda, Chai na gesi asilia inayovunwa na kupelekwa Dar es saalam lakini wananchi wa Rungwe wamekuwa ni masikini wa kutupwa kutokana na uongozi mbovu wa Serikali ya Chama cha Mapinduzi.
''Tumekuwa na wabunge maprofesa Mark Mwandosya na David Mwakyusa kwa muda wa miaka kumi na tano lakini wamekuwa ni mizigo wasio kuwa na huruma kwa wananchi waliowachagua nikiwa mbunge nitareta mabadiriko''alisema.
Mwambigija aliyebatizwa Majina Kama waziri mkuu wa Mbeya na Yohana mbatizaji, alisema akiwa mbunge hatahamia Dar es salaam kama ilivyo kwa wabunge wa chama cha mapinduzi na kuwa atahakikisha anaboresha sekta zote zilizodhorota.

Na Rungwe Yetu




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni