Jumatatu, 2 Februari 2015

NI AJALI MBAYA SANA, HAIJAWAHI KUTOKEA KATIKA WILAYA YA RUNGWE.


Askari Polisi wa wilayani Rungwe wakibeba mwili wa Marehemu Bi Zawadi Mwasongela

 Mwili wa Marehemu wakiupakia katika gari ya Polisi kwa ajili ya kuupeleka
 hospital ya Wilaya ya Rungwe, Makandana kwa ajili ya kuuthibitisha.

 Wanakijiji wa kijiji cha Mwambegele Tukuyu wakishuhudia mwili wa Marehemu Ukipelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Rungwe, Makandana.

 Namba ya Gari iliyohusika na ajali hiyo.

 Mashuhuda wa Ajali hiyo




Ni ajali iliyotokea katika Kijiji cha Mwambegele wilayani Rungwe nje kidogo ya Mji wa Tukuyu barabara kuu iendayo nchi jirani ya Malawi.

Ajali hiyohiyo imehusisha gari aina ya Scania yenye usajili namba T372 BYB, 
Likitokea nchi jirani ya Malawi kwenda Dar es salaam likiwa na shehena ya mbao zenye thamani ya Tsh 50ml.

Mashuhuda wa ajali wanadai kuwa Gari hilo lilishuka mtelemko kwa kasi sana inahisiwa kuwa breki za gari hiyo zilifeli na kupelekea Dereva wa gari hiyo kushindwa kuimudu kona iliyokuwa mbele na kuingia bondeni ambako kuna mto.

Mto huo hutumika na wakazi wa kijiji hicho kwa bahati mbaya sana Bi Zawadi Mwasongela alikuwa katika ujenzi wa nyumba yake alienda mtoni kuteka maji kwa ajili ya ujenzi huo na kukutana na ajali hiyo mbaya iliyokatisha maisha yake. 
marehemu ameacha Mume Watoto 6 na wajukuu 2.

Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina la Bwana libarikiwe Amen!!!!



 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni