Jumanne, 27 Januari 2015

CHAMA CHA MAPINDUZI WILAYA YA RUNGWE KIMEINGIA KATIKA KASFA NZITO BAADA YA KUDAIWA KUUTEKA MSAFARA WA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) NA KUWAJERUHI KWA MAPANGA,MARUNGU NA NONDO.





 Ndg. Max Mwasomola ni Mmoja wa waliojeruhiwa aliyeng'olewa jino na kukatwa kucha
 
 Mwenyekiti wa BAVICHA taifa Ndg. Patrick Ole Sosopi akimtakia hali Max Mwasomola aliyeng'olewa jino na kukatwa kucha na viongozi wa CCM.

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Rungwe Mbeya kimeingia katika kashfa nzito baada ya kudaiwa kuuteka msafara wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  kuwatesa na kuwajeruhi kwa mapanga,rungu na nondo huku wakiwang’oa meno na kucha viongozi watatu wa chadema.

Akizungumza na Tanzania daima leo (jana) kamanda wa ulinzi na usalama wa jimbo la Rungwe Magharibi Reonad Joseph alisema tukio hilo lilitokea saa moja usiku wa kuamkia leo wakiwa njiani wakitokea kata ya Lufilyo walikokuwa wakifanya mkutano.

Alisema Chadema ilikuwa kwenye ziara wilayani humo ambayo iliongozwa na naibu mwenyekiti wa baraza la vijana (BAVICHA) huku Chama cha Mapinduzi wakifanya ziara iliyokuwa chini ya mwenyekiti wao wa mkoa wa Mbeya…… na kwamba wananchi walikuwa mwakisusia mikutano yao na kujaa katika mikutano ya Chadema.

Kutokana na hali hiyo Chama Cha Mapinduzi kupitia makada wake walipanda kuuteka msafara wa viongozi wa Chadema wakati wa kurejea Tukuyu mjini maeneo ya kata ya Mbambo walilazimika kubadirisha njia ili kuwanusuru viongozi wa kitaifa na hatimaye wakafanikiwa kuwateka viongozi watatu waliokuwa na pikipiki.

Aliongeza kuwa baada ya kuwateka viongozi hao walianza kuwapiga na kufanikiwa kuwakata na mapanga maeneo mbalimbali ya sehemu za mwili wao na kuwang’oa meno na kucha  ambapo walikuja okolewa na wananchi wa eneo hilo na hatimaye kuwakimbiza katika hospitali ya wilaya kwa matibabu na kutoa taarifa kwa jeshi la polisi wilayani humo.

Katibu wa siasa itikadi na uenezi wa jimbo hilo,Grece Kalambo alishangazwa na hatua ya Chama hicho kuendesha operesheni hiyo,na kuwa siasa sio ugomvi wanatakiwa kushindana kwa hoja na si kuleta vita pamoja na kuwa wananchi tayari wamekichoka chama hicho wanatakiwa kujitathmini upya.

Mwenyekiti wa jimbo hilo,Juma Kibo alisema chanzo cha Chama hicho kuendesha utekaji kwa viongozi wa chadema ni kutokana na wananchi kususia mikutano yao na kujaa kwenye mikutano ya Chadema kutokana na kuwa na maelezo na sera nzuri zinazowavutia wananchi kila kona.

Kibo aliwataja baadhi ya viongozi waliotekwa na kuteswa kwa kukatwa na mapanga,kung’olewa meno na kucha ni mwenyekiti wa bavicha wilaya,Gastor Mwakasege,aliyepigwa lungu begani na kupokonywa pesa Tsh,laki 2.9 pamoja na simu,Jonathani Mwakyusa aliyekatwa mguu na kupokonywa viatu vyenye thamani ta Tsh,30,000,na Max Mwasomora aliyeng’lewa jino na kucha.

Makamo mwenyekiti wa Baraza la vijana (BAVICHA)Taifa Patrick Olle Sosopi mbali na kushangazwa na tukio hilo alisema utekaji huo ulimlenga yeye na kuwa anaipongeza kamati ya ulinzi na usalama wa jimbo hilo kwa kutambuo hilo na kunibadirishia njia.

Kutokana na hali hiyo Sosopi alilishutumu jeshi la polisi wilayani humo kwa kutowapa ulinzi baada ya kuwapa taarifa juu ya uwepo wa utekaji huo na kwamba majeruhi walipelekwa hospitalini na kwamba wamefungua jarada la kesi nambaTUK/IR/115/2015 shambulio na faili la kesi ni CC NO-9/2015.

Sosopi alisem wameliachia Jeshi la polisi lifanye kazi yake na kuwa kama kutakuwa na upendeleo kwa Chama cha mapinduzi basi watatoa maamuzi magumu juu ya wahusika wote kwa kuwa CCM inakila kitu lakini Chadema wanategemea nguvu ya umma,’’kwa sasa tunaendelea na ziara katika maeneo yote tuliyoyapanga’’alisema.

Mwenyekiti wa umoja wa vijana (UVCCM) wilayani humo,Arbat Kawonga mbali na kukili kuwepo na tukio hilo alisema Chama chake hakihusiki na tukio hilo.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wilayani humo,Ally Mwakalendile alisema yeye hakuwepo wakati tukio hilo likitokea na kuwa hawezi kuzungumza chochote.

Jeshi la polisi wilayani humo limekiri kuepo na tukio hilo na kuwa tayari linamshikilia dereva wa gari aina ya Noah lenye namba T,408 DBM lililotumika kwa shughuri hiyo na kwamba dereva wa gari hilo amepelekwa mahakamani leo na kufunguliwa shitaka hilo.
Mganga mkuu wa hospitali ya wilaya hiyo Dkt,Sungwa Ndagambwe amekiri kupokea majeruhi hao na kuwa wanaendelea kupatiwa matibabu na hali zao zinaendelea vizuri.
Mwisho.

 Na Ibrahim Yassin,Rungwe

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni