Ijumaa, 20 Septemba 2013

UKAGUZI WA MIRADI YA SHULE, HALMASHAURI WILAYA YA RUNGWE, SHULE YA MSINGI MPAKANI.

Wajumbe wa Kamati ya Fedha Utawala na Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe leo wamefanya ukaguzi wa jengo la nyumba ya mwalimu wa Shule ya Msingi Mpakani katika Kata ya Kikole Wilayani Rungwe. Katika siku zote za ukaguzi wa miradi leo wajumbe walikutana na kimbembe cha kutembea zaidi ya Km 15 kwa miguu. Picha chini ni shughuli nzima ya ukaguzi wa Shule ya Mpakani.

 

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Rungwe Mhe. Alfred Mwakasangula katikati akimuaga Makamu Mwenyekiti Mhe. Ezekiel Mwakota kushoto ili aongoze msafara wa safari ya Km 15 kuelekea Shule ya Msingi Mpakani.

 

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Mhe. Ezekiel Mwakota akiwa amewasili Shuleni Mpakani.

 Shule ya Msingi Mpakani kama inavyoonekana katika picha

 Darasa jipya la Shule ya Msingi Mpakani kama linavyoonekana katika picha

Jengo la nyumba ya mwalimu ambayo inajengwa na Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, jengo hili litakapokamilika litaghalimu Shilingi Milioni 15.


Wanafunzi wa darasa la nne na tano kwa pamoja wakiwa katika darasa moja Shuleni Mpakani, Shule hii ina wanafunzi 20, darasa la nne wanafunzi 15, na Darasa la tano wanafunzi 5 Lakini Hali ya madawati ni Mbaya sana.

 

 Wajumbe wa kamati ya Fedha wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe wakiwa chini ya mti tayari kwa kupokea taarifa ya ujenzi wa nyumba ya mwalimu katika Shule ya Msingi Mpakani


 

  Baada ya Kukamilisha shughuli zao kamati hiyo iliondoka hapo Shuleni.



 Wakivuka mito na mabonde kurudi Tukuyu mjini



 Picha na Bashiru Madodi













Hakuna maoni:

Chapisha Maoni