Alhamisi, 28 Januari 2016

Rais Dkt Magufuli Afanya Uteuzi Wa Naibu Gavana Wa Benki Kuu Ya Tanzania


Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, amemteua Ndugu Julian Banzi Raphael, kuwa Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania.

Kabla ya uteuzi huu Ndugu Julian Banzi Raphael alikuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Biashara na Viwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.


Ndugu Julian Banzi Raphael anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Ndugu Juma RELI ambaye muda wake umemalizika tarehe 12 Julai, 2015.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni