Jumatatu, 21 Septemba 2015

MAKAMU WA RAIS MOHAMED GHARIB BILAL AHUDHURIA KUWEKWA WAKFU ASKOFU KENEN PANJA MJINI TUKUYU





 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Abass Kandoro wakati alipowasili kwenye Uwanja wa ndege wa Songwe mkoani humo leo Sept 20,2015 kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuwekwa wakfu Askofu mteule  wa Kanisa la Morovian Tanzania Jimbo la kusini Mchungaji Kenan Salim  Pannja zilizofanyika katika Uwanja wa michezo wa Tandale mjini Tukuyu  Mkoani Mbeya.
  
 
Wasanii wa kwaya ya Kanisa la Morovian Tanzania Jimbo kuu la kusini wakitoa burudani wakati wa sherehe ya kuwekwa wakfu Askofu Kenen Salim Panja iliyofanyika leo Sept 20,2015 katika Uwanja wa michezo wa Tandale mjini Tukuyu  Mkoani Mbeya. 
 
 

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akisalimiana na kumpongeza Askofu mteule wa Kanisa la Morovian Tanzania Jimbo la kusini Mchungaji Kenan Salim  Panja wakati wa sherehe ya kuwekwa wakfu iliyofanyika leo Sept 20,2015 katika Uwanja wa michezo wa Tandale mjini Tukuyu  Mkoani Mbeya.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akiwahutubia waumini wa Kanisa la Morovian Tanzania Jimbo la kusini kwenye sherehe ya kuwekwa wakfu Askofu mteule wa Kanisa hilo Mchungaji Kenan Salim  Panja iliyofanyika leo Sept 20,2015 katika Uwanja wa michezo wa Tandale mkoani Tukuyu Mkoani Mbeya.
 
 

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akiagana na Askofu wa Kanisa la Morovian Tanzania Jimbo la kusini Kenen Salim Panja baada ya kumalizika kwa Misa na Ibada maalum ya kuwekwa wakfu Askofu huyo iliyofanyika leo Sept 20,2015 katika Uwanja wa michezo wa Tandale mjini Tukuyu Mkoani Mbeya.

Jumatano, 26 Agosti 2015

CHAMA Cha Demokrasia na maendeleo(CHADEMA)wilayani Rungwe Mbeya kimezindua kampeni zake leo

 Mgombea Ubunge jimbo la Rungwe Kwa Tiketi ya CHADEMA akiwasalimia wananchi Wa RUNGWE




                                                     
CHAMA Cha Demokrasia na maendeleo(CHADEMA)wilayani Rungwe Mbeya kimezindua kampeni zake leo huku kikimnadi John Mwambigijakuwa mgombea Ubunge jimbo la rungwe magharibi kupitia UKAWA ambaye alitaja vipaumbele kadhaa pindi atakapochaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo.
 
Mwenyekiti wa Chadema jimbo hilo,Juma Kibo alisema chadema haikukosea kumteua Mwambigija kugombea nafasi  hiyo kwa kuwa amekidhi vigezo na anakubarika ndani na nje ya Chama na kuwa endapo wananchi watampa ridhaa ya kuwa mbunge wanauhakika ataondoa kero zilizoshidwa kutolewa na ccm wilayani hapo.

‘’Ushindi wa Ukawa katika uchaguzi wa mwaka huu ni asubuhi kwa kuwa wananchi wanaimani na wagombea watokanao na Ukawa na kuwataka wananchi wachague madiwani,wabunge na Rais ili Chama cha Mapinduzi kiweze kupumzika kwa amani’’alisema  Juma Mwambelo amaye ndiye Mwenyekiti wa chama Wilaya.

Mbunge wa jimbo la Mbeya mjini Joseph Mbilinyi (SUGU)alisema iwapo wananchi watamchagua Mwambigija kuwa mbunge wa jimbo hilo,atashirikiana nae  ilikuhakikisha wanaziondoa kero zote kwa kuwa ccm imeshindwa kuwatumikia wananchi.

Alisema Serikali ya Chama cha mapinduzi imeuza viwanda vyote na kuifanya nchi hii kuwa masikini wa kutupwa na kuwa Ukawa ndiyo tumaini la kweli hasa kuwapata wagombea makini akiwemo wa urais Edwald Lowassa kiongozi makini anayeweza kulikomboa Taifa hili.

kwa upande wake mgombea ubunge wa jimbo hilo John Mwambigija mbali na kuwapongeza wana Rungwe kujitokeza kwa wingi kwenye uzinduzi huo aliouita wa kihistoria alisema hata waangusha wanarungwe na kuwa atahakikisha anakuwa nao bega kwa bega kuhakikisha maendeleo yanapatikana.

Alisema ni haibu kwa wilaya yenye kila kitu lakini imekosa maendeleo kutokana na viongozi watokanao na ccm kutokuwa na hofu ya mungu katika utawala wao na kwamba akichaguliwa kuwa mbunge atahakikisha anaondoa kero za afya,maji,kilimo na masoko,miundombinu ya barabara na kusimamia masrahi ya wafanyakazi.

Nae mgombea Ubunge viti maalum kupitia chama hicho,Jeska Mkumbwa alisema atazunguka kila mahala kuhakikisha wanatoa elimu kwa akina mama ambao wanatajwa kuwa ni mtaji wa ushindi wa ccm ili wasiwe madaraja kwa chama kisichokuwa na misingi ya utawala bora na kuwataka wabadirike.

Wananchi kwa upande wao,walisema wanaimani na wagombea waliosimamishwa na Ukawa wakidai kuwa wamekidhi vigezo vya kuwa viongozi na kusema kuwa watawapa kura za ndiyo kwa kuwa chama cha Mapinduzi kimepoteza muelekeo hasa walipomteua Saul Amon mwenye sifa chafu kuwa mgombea kupia chama hicho.
  





 
MWISHO.

Ijumaa, 14 Agosti 2015

TUKIO LA KUSIKITISHA : RUNGWE AUAWA KINYAMA NA KUTUPWA KADO YA BARABARA





Tukio hilo limetokea wilayani rungwe mkoani Mbeya kata ya Katumba. Marehemu anasadikika kuwa ni mkazi wa Wilayani Ileje Mkoani Mbeya.
Pia inasemekana kuwa marehemu ametupwa sehemu hiyo usiku wa kuamkia leo na watu wasiosemekana  kwa kutumia Usafiri wa bodaboda.
                                     Picha zaidi.










Alhamisi, 30 Julai 2015

PICHA: Lowassa Achukua Fomu ya Urais CHADEMA


Edward Lowassa akionesha fomu ya kuwania urais aliyokabidhiwa leo Makao makuu ya Chadema,D ar.
CLJ5hSGWoAACCU3
Umati wa watu waliojitokeza kumpokea Lowassa wakati akichukua fomu ya urais kupitia Chadema.
CLJ8fhkW8AA6IKB
…Akisaini katika kitabu cha wageni.
CLJ9y4iWEAAZWy7
Mnadhimu Mkuu kambi rasmi ya upinzani bungeni, Tundu Lissu akitoa yake machache.CLJ52JsWwAA--Yc
Lowassa akiwasiri kwenye Ofisi za Makao Makuu ya Chadema, Dar leo.
CLKRw2sWcAAzeL9
Baada ya kuchukua fomu.
mbowe na lowassa
Mwenyekiti wa Chadema (kushoto) Mhe. Freeman Mbowe Mhe. Edward Lowassa (katikati) wakati wa zoezi la kuchukua fomu lililofanyika leo Makao Makuu ya Chadema Kinondoni jijini Dar .
LOWASA (1)
LOWASA (2)
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa akiwa katika meza kuu ya Chadema.
 **
WAZIRI MKUU wa zamani, Mhe. Edward Lowassa hivi punde amechukua fomu ya kuwania nafasi ya urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
 
Lowassa amekabidhiwa fomu hiyo na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe kwenye ofisi za Makao Makuu ya chama hicho yaliyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam.
 
Lowassa alijiunga rasmi na Chadema juzi akitokea CCM baada ya kuondolewa kwenye mchakato wa kuwa mgombea urais wa chama hicho akidai kuwa jina lake liliondolewa kwa mizengwe.

Jumatano, 29 Julai 2015

Job Ndungai amshushia kipigo mgombea mwenza.

Mtia nia wa Jimbo la Kongwa, Dk. Joseph Chilongani akiwa amelazwa hospitali mjini Kongwa
 Mtia nia wa Jimbo la Kongwa, Dk. Joseph Chilongani akiwa amelazwa hospitali mjini Kongwa


NAIBU Spika na Mbunge wa Jimbo la Kongwa Job Ndugai amemshushia kipigo mgombea mwenzake Dk.Joseph Chilongani na kusababishwa kuzirai na kukimbizwa katika hospitali ya Wilaya ya Kongwa. Anaandika Dany Tibason, Kongwa, Dodoma … (endelea).
Ndugai alimpiga kwa fimbo Dk. Chilongani kutokana na kitendo chake cha kutumia simu yake ya mkononi kurekodi matukio ya ubishani baina yao na Saimon Ngatunga.
Akizungumza na gazeti hili, mdogo wa mgombea huyo Michael Chilongani alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 10 jioni katika Kata ya Ugogoni mjini Kongwa wakati wakiwa kwenye kampeni ya kujinadi kwa wanachama.
Amesema ndugu yake huyo amepigwa fimbo kichwani na tumboni na kusababisha kupoteza fahamu kwa zaidi ya saa mbili ambapo alikimbizwa kituo cha polisi kwa ajili ya kupatiwa fomu namba tatu na kisha kupelekwa hospitali.
Ndugai alimshushia kipigo mwenzake baada baada ya mgombea aliyetangulia kudai kwamba iwapo Chama kitampa ridhaa ya kuwania nafasi ya ubunge hatahakikisha anapambana ubadhirifu wa fedha katika halmashauri.
‘Baada ya fahamu kumrudia majira ya saa moja na nusu usiku, kaka alidai anasikia maumivu makali kwenye paji la uso pamoja na kichwani huku akipata shida kuzungumza,’ amesema.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo waliliambia gazeti hili kuwa kabla ya Dk. Chilongani kujeruhiwa kwa fimbo na mgombea mwenzake alitaka kumpiga fimbo hiyo mgombea mwingine aliyejinadi kuwa atakomesha ubadhirifu katika halmashauri ambapo kamati ya ulinzi iliwahi kumzuia.
Naye Kaimu Katibu wa CCM wilaya ya Kongwa Peter Minja amesema kila mgombea ambaye anamalalamiko ayapeleke katika vikao husika.
Kuhusu vurugu za ndugai kumpiga mwenzake amesema mpaka sasa hawajapokea malalamiko yoyote kwa utaratibu unaotakiwa na badala yake wamekuwa wakipokea malalamiko ya maneno.
Alipotafuwa Mkuu wa polisi Mkoa wa Dodoma David Misime alipotakiwa kuzungumzia suala hilo kama amepokea taarifa za Ndugai kumpiga mwenzake amesema hana taarifa .
Amesema hayupo ofisini na akiwa ofisini na kupata taarifa ataweza kuviarifu vyombo vya habari.
NAIBU Spika na Mbunge wa Jimbo la Kongwa Job Ndugai amemshushia kipigo mgombea mwenzake Dk.Joseph Chilongani na kusababishwa kuzirai na kukimbizwa katika hospitali ya Wilaya ya Kongwa.
Ndugai alimpiga kwa fimbo Dk.Chilongani kutokana na kitendo chake cha kutumia simu yake ya mkononi kurekodi matukio ya ubishani baina yao na Saimon Ngatunga.
Akizungumza na gazeti hili, mdogo wa mgombea huyo Michael Chilongani alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 10 jioni katika Kata ya Ugogoni mjini Kongwa wakati wakiwa kwenye kampeni ya kujinadi kwa wanachama.
Amesema ndugu yake huyo amepigwa fimbo kichwani na tumboni na kusababisha kupoteza fahamu kwa zaidi ya saa mbili ambapo alikimbizwa kituo cha polisi kwa ajili ya kupatiwa fomu namba tatu na kisha kupelekwa hospitali.
Ndugai alimshushia kipigo mwenzake baada baada ya mgombea aliyetangulia kudai kwamba iwapo Chama kitampa ridhaa ya kuwania nafasi ya ubunge hatahakikisha anapambana ubadhirifu wa fedha katika halmashauri.
‘Baada ya fahamu kumrudia majira ya saa moja na nusu usiku, kaka alidai anasikia maumivu makali kwenye paji la uso pamoja na kichwani huku akipata shida kuzungumza,’ amesema.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo waliliambia gazeti hili kuwa kabla ya Dk. Chilongani kujeruhiwa kwa fimbo na mgombea mwenzake alitaka kumpiga fimbo hiyo mgombea mwingine aliyejinadi kuwa atakomesha ubadhirifu katika halmashauri ambapo kamati ya ulinzi iliwahi kumzuia.
Naye Kaimu Katibu wa CCM wilaya ya Kongwa Peter Minja amesema kila mgombea ambaye anamalalamiko ayapeleke katika vikao husika.
Kuhusu vurugu za ndugai kumpiga mwenzake amesema mpaka sasa hawajapokea malalamiko yoyote kwa utaratibu unaotakiwa na badala yake wamekuwa wakipokea malalamiko ya maneno.
Alipotafuwa Mkuu wa polisi Mkoa wa Dodoma David Misime alipotakiwa kuzungumzia suala hilo kama amepokea taarifa za Ndugai kumpiga mwenzake amesema hana taarifa .
Amesema hayupo ofisini na akiwa ofisini na kupata taarifa ataweza kuviarifu vyombo vya habari.

Jumanne, 28 Julai 2015

CCM KUMJIBU LOWASSA LEO


Wednesday, July 29, 2015

CCM Kumjibu LOWASSA Leo


Baada ya Mbunge wa Monduli Edward Lowassa kutangaza kuhama Chama Cha Mapinduzi (CCM)  na kuhamia Chadema jana katika ukumbi wa Bahari Beachi jijini Dar es salaam, chama cha Mapinduzi kimetoa taarifa ya kuzungumza na Vyombo vya Habari  leo.
 
Taarifa hiyo ya chama cha Mapinduzi haijafafanua kuwa ajenda itakuwa nini katika kikao hicho lakini kwa mujibu wa watafiti wa masuala ya kisiasa wanasema kuwa kikao hicho kitakuwa maalumu kwa ajili ya kujibu shutuma zilizotolewa na Lowassa kuhusiana na madai ya kuwepo uonevu wakati akiomba ridhaa ya kupeperusha Bendera ya CCM.
 
Mtandao huu utakujulisha kitakachojiri katika mkutano huo.



Jumatatu, 27 Julai 2015

Lowasa ajiunga rasmi CHADEMA




BREAKING NEWS : LOWASA AJIUNGA CHADEMA RASMI, PICHA NA VIDEO ZA KILICHOONGELEWA LEO NMEKUWEKEA 

 


Lowassa Akaribishwa Rasmi UKAWA......

 

“Watanzania wanataka mabadiliko, wasipoyapata ndani ya CCM watayatafuta nje”. Hii ni moja ya kauli  ambayo Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli, Edward Ngoyai Lowassa aliziongea Arusha May 30 2015 alipotangaza nia ya Kugombea Urais kupitia CCM.
 
CCM ilikuwa na Wagombea zaidi ya 40 ambao walitangaza nia na kuchukua fomu za Kugombea Urais 2015 lakini baadae Chama hicho kikampitisha Dk. John Pombe Magufuli kugombea nafasi hiyo, baada ya hapo kukawa na  taarifa nyingi sana kuhusu ishu ya Edward Lowassa na UKAWA.
 
Viongozi wa Umoja wa UKAWA wamekutana Dar  leo  na mmoja wa Viongozi hao, James Mbatia amesema wamekubaliana kumkaribisha Mbunge Edward Lowassa ndani ya UKAWA na wako tayari kumpa nafasi na kushirikiana nae.

Mbatia  ameongeza kuwa Lowassa ni mchapa kazi makini na mfuatiliaji wa karibu wa kiutendaji katika majukumu anayokabidhiwa.
 
Alipoulizwa kuwa Lowassa atakuwa mgombea Urais Mbatia amesema kila chama kina utaratibu wake  hivyo mchakato ukishakamilika  atatangazwa mgombea urais wa UKAWA mmoja  mwanzoni mwa mwezi agosti.