Jumatatu, 1 Juni 2015

MH. PROFESA JAMES MARK MWANDOSYA ATANGAZA NIA YA KUOMBA KUWANIA URAIS KWA TIKETI YA CHAMA CHA MAPINDUZI. KAULI MBIU NI KWA PAMOJA TUTAIJENGA TANZANIA TUNAYOITAKA.

Wafuasi wa Profesa Mwandosya wakiingia na mabango kwenye uwanja wa tukio

Profesa Mwandosya pamoja na familia yake wakiwasili eneo la tukio

Profesa Mwandosya pamoja na Mke wake wakipiga makofi mara baada ya kuwasili eneo la mkutano

Mke wa Profesa Mwandosya Bi Lucy Mwandosya akiwasalimia wananchi




Wananchi wakiwa wamefurika katika eneo la mkutano kumsikiliza Profesa Mwandosya akitangaza nia ya kugombea uraisi

Jumatatu, 25 Mei 2015

Madiwani Walia Na Ndoa FEKI Za Walimu......Wadai Upungufu Wa Walimu Vijijini Unasababishwa Na Walimu Wa Kike Kughushi Vyeti Vya Ndoa


BAADHI ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, mkoani Tanga, wamesema tatizo la upungufu wa walimu kwenye shule za msingi zilizopo vijijini kunachangiwa na walimu hasa wa kike kutaka kufundisha mjini.

Walisema baadhi ya walimu wa kike wamekuwa wakighushi vyeti vya ndoa ili kuonesha wameolewa na kuwafuata waume zao mijini jambo linalozorotesha jitihada za Serikali kumaliza tatizo la walimu kwani baadhi ya shule za vijijini zina walimu hadi wawili.

Madiwani hao waliyasema hayo mwishoni mwa wiki kwenye Kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo Diwani wa Kata ya Lusanga, Sesiwa Mhando, alidai halmashauri ilitenga sh. milioni 30 kwa ajili ya walimu kupelekwa shule za vijijini; lakini hadi sasa hajui mchakato huo umekwamia wapi.

"Tatizo la walimu kwenye shule za msingi linatokana na walimu kujazana mijini hasa wa kike wakiwa na ndoa   bandia, madiwani tulitenga sh. milioni 30 ili zitumike kupeleka walimu vijijini lakini sijui mchakato huo umeishia wapi," alihoji.

Kwa upande  wake, Kaimu Ofisa Elimu wa Shule za Msingi wilayani humo, Stuart Kuziwa, alisema tatizo la walimu ni la kitaifa likiwemo la kujazana mijini lakini hata shule zilizopo mjini nazo zina upungufu wa walimu.

"Hata shule za mjini nazo zina upungufu wa walimu, tumeomba kupatiwa walimu 230 kwa miaka mitatu mfululizo, hilo linaweza kumaliza shida ya walimu katika shule za msingi," alisema.

Diwani wa Kata ya Bwembera, Kapteni mstaafu Tito Haji, alisema moja ya shule za msingi kwenye kata yake ina walimu wawili.

"Kwenye Kamati ya Fedha,mlidai tatizo la walimu limekwisha sasa iweje leo mnatueleza kuwa tatizo la walimu bado lipo Muheza, Shule ya Msingi Msowelo ina walimu wawili lakini mjini walimu wamejaa," alisema Kapteni Tito.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Amir Kiroboto, alisema madiwani wasilalamikie tatizo la walimu kujaa mijini bali waangalie idadi ya wanafunzi kwani shule nyingi za mjini zina wanafunzi wengi.

Edward Lowassa Aongea na Vyombo vya Habari LEO....... Adai hahusiki na Kashfa ya Richmond, Hana Mpango wa Kuhama CCM na Yupo Tayari Kupima Afya


Waziri Mkuu mstaafu  Edward Lowassa leo amefanya  mkutano maalum nyumbani kwake mjini Dodoma  na  wahariri  wakuu  wa  vyombo  mbalimbali  vya  habari  hapa  nchini. Katika mkutano huo kwa ufupi Lowassa amesema yafuatayo;

1. Amesema Hahusiki lolote na sakata la Richmond na ndio sababu hata kamati ya Mwakyembe haikuona sababu ya kumhoji.
 
 Amesisitiza kuwa cheo cha uwaziri mkuu ndio ilikuwa lengo la kamati ya mwakyembe na spika wa bunge kipindi hicho Samwel Sitta.
 
Amesisitiza hicho sio kikwazo kwake katika kuingia Ikulu kwani sakata la Richmond lilipikwa kumchafua. Amechukua muda mrefu kuzungumzia hili la Richmond na amesema atalisema zaidi Arusha wikendi hii.(Jumamosi)

2. Anaamini kila mtangaza nia ana makundi ya kumuunga mkono. Yeye katika mkutano huu na wahariri leo ameambatana na Nazir Karamagi, Peter serukamba, Diana chilolo, Hussein Bashe na wengineo .
 
Pia aliyekuwa mkurugenzi wa HakiElimu Elizabeti Misoki ametangazwa rasmi kuwa Mkurugenzi wa mahusiano na mawasiliano katika timu ya kampeni ya Lowassa. Amehoji kwani akina Karamagi wana tatizo gani na kwani wao sio binadamu?

3. Lengo kuu atakaloanza nalo ni Elimu na sio Kilimo kwanza . Amesema serikali ya JK ilikosea kuanza na kilimo na kuweka kando elimu. Ametangaza kuwa sera yake ni Elimu Kwanza.

4. Kuhusu pesa anasema anapata michango ya rafiki zake na ataendelea kupokea michango hii wakati wote wa harakati zake na haina madhara yotote.

5. Anasema hatahama CCM na asiyemtaka yeye CCM ndie aondoke ndani ya chama kwani yeye ana uhakika wa kupata nafasi kuwania urais.

6. Amesema hatalipa kisasi kwa lolote lililomtokea katika siasa. Amemwachia Mungu kwani yeye ni mcha Mungu.

7. Amesema Arusha itawaka moto tarehe 30 mwezi huu na kuwataka watanzania kutega sikio kwani ataanika kila jambo kuhusu mustakabali wa nchi hii na mipango yake ya kuiinua nchi kiuchumi katika miaka kumi ijayo.

Ijumaa, 15 Mei 2015

MKUU WA WILAYA YA RUNGWE MWL. ZAINABU MBUSI AFUNGUA MRADI WA UENDELEZAJI WA SEKTA YA MAZIWA AFRIKA MASHARIKI ULIOANZISHWA WIRAYANI RUNGWE

 Mkuu wa wilaya ya Rungwe Mwl. Zainabu Mbusi Akiwahutubia wafugaji wa Ng'ombe Katika viwanja vya Shule ya Msingi Salemu Kyimo (K.K)


 Katibu Tawala Ndg. Moses Mashaka Akisoma taarifa kwa mkuu wa Wilaya ya Rungwe


  Mwl Elizabeth Sekile

 Diwani wa Kata ya Bulyaga Mhe. Mwalusamba Akiongea kwa niaba ya Waheshimiwa Madiwani wenzake.

 Mkuu wa Wilaya akijaza fomu ya Kujiunga na Mradi huo nakuwahamasisha wafugaji wengi kujiunga

 Akionesha Risiti aliyolipia pesa ya kujiunga.


 Wafugaji wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya Akihutubia

 Mkuu wa Wilaya akilisakata Kwaito wakati wa kufunga Mkutano huo.




Mkuu wa Wilaya ya Rungwe  Mwl. Zainabu Mbusi amesema kuwa itolewe elimu kwa vijana juu ya ufugaji wa Ng'ombe wa maziwa ili kujipatia ajira ya kudumu ili kuepuka dhana ya kutegemea kuajiliwa na serikali.
Na amesisitiza kuwa ziteuliwe shule za sekondari kwa ajili ya kuwapa elimu ya kujitegemea vijana baada ya kuhitimu masomo yao.

alitoa lai kwamba kuna tabia mbaya sana inayopelekea wananchi wa Rungwe kuwa masikini sana, tabia ya kuchumbia Migomba ya Ndizi na kusisitiza kuwa ikomeshwe mala moja na badala yake wananchi wafuge Ng'ombe wa Maziwa ili kujikwamua na lindi la umasikini na kuachana na tabia ya kuchumbia Ndizi.


MAPINDUZI YAFELI BURUNDI NA MAJENERALI WAWILI WALIOFANYA JARIBIO HILO WAKAMATWA

MAPINDUZI YAFELI BURUNDI

Mnamo 13 mwezi May jenerali mmoja wa jeshi alitangaza katika redio ya taifa kwamba rais wa Burundi amepinduliwa na kwamba serikali ya mpito itabuniwa.Lakini msemaji wa rais alikana habari hizo akidai kuwa kulikuwa na usaidizi mdogo katika jeshi kwa mapinduzi kutendeka.
18.00-makaribisho ya Nkurunziza

Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza ametuma ujumbe katika mtandao wake wa tweetter kwa lugha ya kirundi akisema kuwa ''Nilifurahi kuona vile raia wa Burundi walivyonipokea katika mji wa Bujumbura pamoja na mikoa mingine
17.45pm-Hofu yatanda Burundi
Wafuasi wa Nkurunziza mjini Bujumbura
Kuna mazingira ya hofu na switofahamu katika mji wa Bujumbura kufuatia kufeli kwa jaribo la mapinduzi kulingana na mkaazi mmoja wa mji huo.Serge Ntabikiyoboka anasema kuwa hadhani kwamba taifa hilo literejea katika hali yake ya kawaida hivi karibuni.

17.30-UN ina wasiwasi kuhusu Burundi.
Tume ya haki za binaadamu katika umoja wa mataifa imeonya kuhusu ulipizaji kisasi kufuatia jaribio la mapinduzi nchini Burundi.Msemaji wake Rupert Coleville amesema kuwa tume hiyo ina wasiwasi kuhusu matukio ya taifa hilo katika kipindi cha siku mbili zilizopita.
16.20pm-Nurunziza awasili Bujumbura
 
Rais Pierre Nkurunziza amewasili katika makao ya rais mjini Bujumbura kupitia msafara mkubwa wa magari .Alikaribishwa na umati mkubwa wa wanachama wa chama chake ambao walikuwa wamevaa mavazi ya bendera za chama hicho huku wakicheza densi.
16.10pm-wafuasi wa Nkurunziza
Mwandishi wa BBC Ruth Nesoba ametuma picha za wafuasi wa rais Pierre Nkurunziza kufuatia kuwasili kwa rais huyo katika ,mji mkuu wa Bujumbura
16.00pm-wanajeshi walioasi
Baadh ya picha za askari waasi wa jaribio la mapinduzi
Baadhi ya picha za wanajeshi waasi waliohusika na jaribio la mapinduzi nchini Burundi ambao wamekamatwa
13.30-Raia wamlaki rais Ngozi
wafuasi wa rais Pierre Nkurunziza
Mashahidi wameiambia BBC kwamba rais Pierre Nkurunziza amerudi kwao huko Ngozi nchini Burundi na amekuwa akiendeshwa katika gari lilo wazi upande wa juu na kwamba raia wamemlaki kwa shangwe na vigelegele
13.23pm-Nkurunziza arudi nyumbani kwake Ngozi
Rais Pierre Nkurunziza
Shirika la habari la AFP limeripoti kwamba rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amerudi nyumbano kwao huko Ngozi yapata kilomita 140 kazkazini mwa mji mkuu wa Bujumbura kulingana na duru ambazo hazikutaka kujulikana zilizo karibu na kiongozi huyo.''Aliwasili katika eneo la Ngozi siku ya Alhamisi.Ni hapa ambapo anatarajiwa kulihutubia taifa kuhusu jaribio la mapinduzi lililofeli'',.AFP lilimnukuu aliyetoa habari hizo.
12.00-Raia watakiwa kuendeleza maandamano
Maandamano Burundi
Kiongozi wa kundi la kiraia linalopinga hatua ya rais Nkurunziza kuwania muhula wa tatu amewataka raia nchini humo kuendelea na maandamano kulingana na shirika la habari la AFP.
Vital Nshimiriman amesema kuwa licha ya kundi hilo kupinga jaribio hilo la mapinduzi,vile raia walivyowashangilia wanajeshi wa jaribio hilo kulionyesha kwamba kuna hamu kubwa ya mabadiliko.
10.30am-Majenerali waasi kushtakiwa
Nukuu muhimu kutoka kwa Gervais Abayeho,msemaji wa rais Pierre Nkurunziza akizungumza na kipindi cha BBC cha Newsday.''Mapinduzi hushirikisha watu wengi Kuna wanajeshi wa nyadhfa za chini ambao wamesalimu amri na ambao wanawasaidia maafisa wa poisi na uchunguzi wao,lakini ninaamini watu waliopanga mapinduzi hayo ,wale viongozi hilo ni swala jingine ni lazima washtakiwe.hakuna mgawanyiko katika jeshi.Iwapo unaweza kuwaangalia wale waliokuwa wakipanga kutekeleza mapinduzi ni wachache ...kundi dogo la jeshi'',alisema..
Majenerali wawili waliotekeleza jaribio la mapinduzi nchini Burundi dhidi ya rais Pierre Nkurunziza wamekamatwa.
Hatahivyo kiongozi wa mapinduzi hayo jenerali Godefroid Niyombare ametoroka na anasakwa kulingana na msemaji wa rais.
Awali Jenerali Niyombare alikiambia chombo cha habari cha AFP kwamba yeye na wafuasi wake watajisalimisha akiongezea kuwa ''natumai hawatatuua''.
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amesema kuwa amerudi nchini Burund na kwamba anatarajiwa kulihutubia taifa.