BAADHI
ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, mkoani Tanga, wamesema
tatizo la upungufu wa walimu kwenye shule za msingi zilizopo vijijini
kunachangiwa na walimu hasa wa kike kutaka kufundisha mjini.
Walisema
baadhi ya walimu wa kike wamekuwa wakighushi vyeti vya ndoa ili
kuonesha wameolewa na kuwafuata waume zao mijini jambo linalozorotesha
jitihada za Serikali kumaliza tatizo la walimu kwani baadhi ya shule za
vijijini zina walimu hadi wawili.
Madiwani
hao waliyasema hayo mwishoni mwa wiki kwenye Kikao cha Baraza la
Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo Diwani wa Kata ya Lusanga, Sesiwa
Mhando, alidai halmashauri ilitenga sh. milioni 30 kwa ajili ya walimu
kupelekwa shule za vijijini; lakini hadi sasa hajui mchakato huo
umekwamia wapi.
"Tatizo
la walimu kwenye shule za msingi linatokana na walimu kujazana mijini
hasa wa kike wakiwa na ndoa bandia, madiwani tulitenga sh. milioni 30
ili zitumike kupeleka walimu vijijini lakini sijui mchakato huo umeishia
wapi," alihoji.
Kwa
upande wake, Kaimu Ofisa Elimu wa Shule za Msingi wilayani humo,
Stuart Kuziwa, alisema tatizo la walimu ni la kitaifa likiwemo la
kujazana mijini lakini hata shule zilizopo mjini nazo zina upungufu wa
walimu.
"Hata
shule za mjini nazo zina upungufu wa walimu, tumeomba kupatiwa walimu
230 kwa miaka mitatu mfululizo, hilo linaweza kumaliza shida ya walimu
katika shule za msingi," alisema.
Diwani wa Kata ya Bwembera, Kapteni mstaafu Tito Haji, alisema moja ya shule za msingi kwenye kata yake ina walimu wawili.
"Kwenye
Kamati ya Fedha,mlidai tatizo la walimu limekwisha sasa iweje leo
mnatueleza kuwa tatizo la walimu bado lipo Muheza, Shule ya Msingi
Msowelo ina walimu wawili lakini mjini walimu wamejaa," alisema Kapteni Tito.
Mwenyekiti
wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Amir Kiroboto, alisema madiwani
wasilalamikie tatizo la walimu kujaa mijini bali waangalie idadi ya
wanafunzi kwani shule nyingi za mjini zina wanafunzi wengi.
Waziri
Mkuu mstaafu Edward Lowassa leo amefanya mkutano maalum nyumbani
kwake mjini Dodoma na wahariri wakuu wa vyombo mbalimbali vya
habari hapa nchini. Katika mkutano huo kwa ufupi Lowassa amesema
yafuatayo;
1. Amesema Hahusiki lolote na sakata la Richmond na ndio sababu hata kamati ya Mwakyembe haikuona sababu ya kumhoji. Amesisitiza kuwa cheo cha uwaziri mkuu ndio ilikuwa lengo la kamati ya mwakyembe na spika wa bunge kipindi hicho Samwel Sitta. Amesisitiza
hicho sio kikwazo kwake katika kuingia Ikulu kwani sakata la Richmond
lilipikwa kumchafua. Amechukua muda mrefu kuzungumzia hili la Richmond
na amesema atalisema zaidi Arusha wikendi hii.(Jumamosi)
2.
Anaamini kila mtangaza nia ana makundi ya kumuunga mkono. Yeye katika
mkutano huu na wahariri leo ameambatana na Nazir Karamagi, Peter
serukamba, Diana chilolo, Hussein Bashe na wengineo . Pia
aliyekuwa mkurugenzi wa HakiElimu Elizabeti Misoki ametangazwa rasmi
kuwa Mkurugenzi wa mahusiano na mawasiliano katika timu ya kampeni ya
Lowassa. Amehoji kwani akina Karamagi wana tatizo gani na kwani wao sio
binadamu?
3.
Lengo kuu atakaloanza nalo ni Elimu na sio Kilimo kwanza . Amesema
serikali ya JK ilikosea kuanza na kilimo na kuweka kando elimu.
Ametangaza kuwa sera yake ni Elimu Kwanza.
4.
Kuhusu pesa anasema anapata michango ya rafiki zake na ataendelea
kupokea michango hii wakati wote wa harakati zake na haina madhara
yotote.
5.
Anasema hatahama CCM na asiyemtaka yeye CCM ndie aondoke ndani ya chama
kwani yeye ana uhakika wa kupata nafasi kuwania urais.
6. Amesema hatalipa kisasi kwa lolote lililomtokea katika siasa. Amemwachia Mungu kwani yeye ni mcha Mungu.
7.
Amesema Arusha itawaka moto tarehe 30 mwezi huu na kuwataka watanzania
kutega sikio kwani ataanika kila jambo kuhusu mustakabali wa nchi hii na
mipango yake ya kuiinua nchi kiuchumi katika miaka kumi ijayo.
Diwani wa Kata ya Bulyaga Mhe. Mwalusamba Akiongea kwa niaba ya Waheshimiwa Madiwani wenzake.
Mkuu wa Wilaya akijaza fomu ya Kujiunga na Mradi huo nakuwahamasisha wafugaji wengi kujiunga
Akionesha Risiti aliyolipia pesa ya kujiunga.
Wafugaji wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya Akihutubia
Mkuu wa Wilaya akilisakata Kwaito wakati wa kufunga Mkutano huo.
Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Mwl. Zainabu Mbusi amesema kuwa itolewe elimu kwa vijana juu ya ufugaji wa Ng'ombe wa maziwa ili kujipatia ajira ya kudumu ili kuepuka dhana ya kutegemea kuajiliwa na serikali.
Na amesisitiza kuwa ziteuliwe shule za sekondari kwa ajili ya kuwapa elimu ya kujitegemea vijana baada ya kuhitimu masomo yao.
alitoa lai kwamba kuna tabia mbaya sana inayopelekea wananchi wa Rungwe kuwa masikini sana, tabia ya kuchumbia Migomba ya Ndizi na kusisitiza kuwa ikomeshwe mala moja na badala yake wananchi wafuge Ng'ombe wa Maziwa ili kujikwamua na lindi la umasikini na kuachana na tabia ya kuchumbia Ndizi.
Mnamo 13 mwezi May
jenerali mmoja wa jeshi alitangaza katika redio ya taifa kwamba rais wa
Burundi amepinduliwa na kwamba serikali ya mpito itabuniwa.Lakini
msemaji wa rais alikana habari hizo akidai kuwa kulikuwa na usaidizi
mdogo katika jeshi kwa mapinduzi kutendeka.
18.00-makaribisho ya Nkurunziza
Rais
wa Burundi Pierre Nkurunziza ametuma ujumbe katika mtandao wake wa
tweetter kwa lugha ya kirundi akisema kuwa ''Nilifurahi kuona vile raia
wa Burundi walivyonipokea katika mji wa Bujumbura pamoja na mikoa
mingine
17.45pm-Hofu yatanda Burundi
Wafuasi wa Nkurunziza mjini Bujumbura
Kuna mazingira ya hofu na
switofahamu katika mji wa Bujumbura kufuatia kufeli kwa jaribo la
mapinduzi kulingana na mkaazi mmoja wa mji huo.Serge Ntabikiyoboka
anasema kuwa hadhani kwamba taifa hilo literejea katika hali yake ya
kawaida hivi karibuni.
17.30-UN ina wasiwasi kuhusu Burundi.
Tume ya haki za binaadamu
katika umoja wa mataifa imeonya kuhusu ulipizaji kisasi kufuatia jaribio
la mapinduzi nchini Burundi.Msemaji wake Rupert Coleville amesema kuwa
tume hiyo ina wasiwasi kuhusu matukio ya taifa hilo katika kipindi cha
siku mbili zilizopita.
16.20pm-Nurunziza awasili Bujumbura
Rais Pierre Nkurunziza
amewasili katika makao ya rais mjini Bujumbura kupitia msafara mkubwa wa
magari .Alikaribishwa na umati mkubwa wa wanachama wa chama chake ambao
walikuwa wamevaa mavazi ya bendera za chama hicho huku wakicheza densi.
16.10pm-wafuasi wa Nkurunziza
Mwandishi wa BBC Ruth Nesoba
ametuma picha za wafuasi wa rais Pierre Nkurunziza kufuatia kuwasili kwa
rais huyo katika ,mji mkuu wa Bujumbura
16.00pm-wanajeshi walioasi
Baadh ya picha za askari waasi wa jaribio la mapinduzi
Baadhi ya picha za wanajeshi waasi waliohusika na jaribio la mapinduzi nchini Burundi ambao wamekamatwa
13.30-Raia wamlaki rais Ngozi
wafuasi wa rais Pierre Nkurunziza
Mashahidi wameiambia BBC kwamba
rais Pierre Nkurunziza amerudi kwao huko Ngozi nchini Burundi na
amekuwa akiendeshwa katika gari lilo wazi upande wa juu na kwamba raia
wamemlaki kwa shangwe na vigelegele
13.23pm-Nkurunziza arudi nyumbani kwake Ngozi
Rais Pierre Nkurunziza
Shirika la habari la AFP
limeripoti kwamba rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amerudi nyumbano
kwao huko Ngozi yapata kilomita 140 kazkazini mwa mji mkuu wa Bujumbura
kulingana na duru ambazo hazikutaka kujulikana zilizo karibu na kiongozi
huyo.''Aliwasili katika eneo la Ngozi siku ya Alhamisi.Ni hapa ambapo
anatarajiwa kulihutubia taifa kuhusu jaribio la mapinduzi
lililofeli'',.AFP lilimnukuu aliyetoa habari hizo.
12.00-Raia watakiwa kuendeleza maandamano
Maandamano Burundi
Kiongozi wa kundi la kiraia
linalopinga hatua ya rais Nkurunziza kuwania muhula wa tatu amewataka
raia nchini humo kuendelea na maandamano kulingana na shirika la habari
la AFP.
Vital Nshimiriman amesema kuwa licha ya kundi hilo kupinga
jaribio hilo la mapinduzi,vile raia walivyowashangilia wanajeshi wa
jaribio hilo kulionyesha kwamba kuna hamu kubwa ya mabadiliko.
10.30am-Majenerali waasi kushtakiwa
Nukuu muhimu kutoka kwa Gervais
Abayeho,msemaji wa rais Pierre Nkurunziza akizungumza na kipindi cha
BBC cha Newsday.''Mapinduzi hushirikisha watu wengi Kuna wanajeshi wa
nyadhfa za chini ambao wamesalimu amri na ambao wanawasaidia maafisa wa
poisi na uchunguzi wao,lakini ninaamini watu waliopanga mapinduzi hayo
,wale viongozi hilo ni swala jingine ni lazima washtakiwe.hakuna
mgawanyiko katika jeshi.Iwapo unaweza kuwaangalia wale waliokuwa
wakipanga kutekeleza mapinduzi ni wachache ...kundi dogo la
jeshi'',alisema..
Majenerali wawili waliotekeleza jaribio la mapinduzi nchini Burundi dhidi ya rais Pierre Nkurunziza wamekamatwa.
Hatahivyo kiongozi wa mapinduzi hayo jenerali Godefroid Niyombare ametoroka na anasakwa kulingana na msemaji wa rais.
Awali
Jenerali Niyombare alikiambia chombo cha habari cha AFP kwamba yeye na
wafuasi wake watajisalimisha akiongezea kuwa ''natumai hawatatuua''.
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amesema kuwa amerudi nchini Burund na kwamba anatarajiwa kulihutubia taifa.