Ijumaa, 13 Machi 2015

AJARI NYINGINE TENA :BASI LA ARUSHA EXPRESS LAPATA AJALI MBAYA YA KUGONGANA NA LORI


Ajali Arusha: Imetokea ajali ikilihusisha basi la Arusha Express Lenye namba za usajili T 206 BEF na Lori baada ya dereva wa basi kujaribu ku-overtake na kukutana na lori mbele yake






- Hakuna vifo isipokuwa abiria wa Lori ndio wameumia na kukimbizwa Hospitali, na basi hilo lilikuwa likitoka Arusha Kuelekea jijini Mbeya leo asubuhi

taarifa zaidi utazidi kuzipata hapa hapa

Jumatano, 11 Machi 2015

TUKIO KATIKA PICHA NA TAARIFA YA AWALI KUTOKA JESHI LA POLISI MKOA WA IRINGA KUTOKANA NA AJALI YA BASI LA ABIRIA NA LORI ILIYOTOKEA MAPEMA LEO .

 Mashuhuda wa ajali hiyo wakijaribu kuokoa mizigo


 kikosi cha uokoaji wakiwa katika harakati za kulitoa kontena juu ya basi na kutoa miili ya marehemu
 Winchi zikilitoa kontena juu ya basi
 Muonekano wa basi hilo Baada ya kulitoa kontena juu 



 Taarifa za awali kutoka jeshi la polisi mkoani Iringa zinaeleza kuwa basi la kampuni Majinja lenye usajili wa namba T438 CDE lililolaliwa na Lori lilikuwa limebeba jumla ya watu 49, idadi hiyo ni pamoja na dereva na kondakta wa basi hilo.wengi wa watu hao wamefariki dunia idadi ya majeruhi haijajulikana bado. 

 Taarifa hizo zinaeleza kuwa kwenye mizigo mingi ya abiria waliokuwa kwenye basi hilo kumepatikana madaftari mengi ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salaam hivyo jeshi hilo linaendelea kufanya mawasoliano ma wamiliki wa gari hilo ili kujua kama lilikuwa limekodishwa kubeba wanafunzi wa chuo hicho ama ni mchanganyiko wa kawaida wa abiria.

Ajali imetokea changalawe Mafinga



Breaking News:  kwa Taarifa tulizopokea muda huu na ambazo hazijathibitishwa kuwa Basi la Majinja Limepata ajali eneo la Mafinga likitokea Mbeya na inahofiwa watu wengi kupoteza maisha. chanzo mpaka sasa inasemekana ni Lori lilikuwa linakwepa mashimo ,na ndipo likagongana uso kwa uso na Basi hilo Taarifa kamili na Tukio katika Picha zitafuata mara baada ya kupata uhakika kamili endelea kufuatilia hapa, Tayari Kikosi kazi cha Blogs ya rungwe yetu kipo eneo la tukio.

Hawa ni Baadhi ya Merehemu waliokwama katika basi wanaohofiwa kufa katika ajali hiyo

 Nusu ya basi likiwa limepondwa na kontena


Watu wapatao 50 wanahofiwa kufa papo hapo baada ya basi hilo la Majinja Express kugongana na lori na kuangukiwa na kontena

Jumatatu, 9 Machi 2015

Hatari Mtoto mwingine Albino akatwa mkono


       Watoto Albino wamekuwa wakifanyiwa vitendo vya kikatili na kuuawa Tanzania 
Matukio ya ukatili dhidi ya albino yanaendelea kuwa tishio nchini Tanzania baada ya mtoto wa miaka sita kukatwa kiganja cha mkono
Shambulio hilop jipya limetokea mkoani Rukwa kusini magharibi mwa nchi hiyo.
Mtoto huyo kiume Baraka Cosmas alikuwa amelala na mama yake mzazi wakati wahalifu hao walipovamia nyumba yao.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Rukwa Jackob Mwaruanda amesema kwa sasa mtoto huyo anapata matibabu hospitali na hali yake inaendelea vizuri.
Polisi inaendelea na uchunguzi kubaini wahusika.
Shambulio hilo linajitokeza wiki moja tu baada ya watuhumiwa wanne kuhukumiwa adhabu ya kifo kwa mauaji ya albino, Na muda mfupi baada ya Rais Tanzania Jakaya Kikwete kukemea mauaji ya albino, ambao viungo vyao hutumika katika shughuli za kishirikina kwa imani potofu kuwa zinasaidia kuleta utajiri na madaraka.

Jumatano, 4 Machi 2015

MKUU WA MKOA WA MBEYA KANDORO AWAAPISHA WAKUU WAPYA WA WILAYA MBEYA


 Wageni waalikwa waliohudhuria hafla fupi ya kuwaapisha wakuu wa Wilaya Wapya iliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Mbeya jijini hapa.
 Pichani ni wakuu wa Wilaya  za Mkoa wa mbeya

 Kiongozi wa dini ya kiislam akisomna dua katika hafla hiyo

 Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Zainabu Mbussi akiapa mbele ya mkuu wa Mkoa wa Mbeya 
 Mkuu wa Wilaya ya Mbozi Ahmad Nammohe 
 Mkuu wa Wilaya ya Kyela Thea Ntara
 Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Nyerembe Munasa akizungumza kwa niaba ya wenzake 
 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akiwa katika picha ya pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa 
 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa dini.

Jumatatu, 2 Machi 2015

MPYAA MSANII WA BONGO MOVIE MWANADADA CHUCHU AZIRAI NDANI YA JENEZA WAKATI WA KUSHUTI MOVIE


HII ni kali ya mwaka! Staa wa sinema za Bongo, Chuchu Hans amejikuta akizirai ndani ya jeneza wakati akiigiza sini ya kifo kwenye filamu, Amani limeinyaka.
Staa wa sinema za Bongo, Chuchu Hans akiwa kwenye jeneza.
Chuchu alikumbwa na hali hiyo hivi karibuni akiwa ‘lokesheni’ ya kuigizia filamu hiyo maeneo ya Mbezi ya Kimara jijini Dar es Salaam ambapo sanjari na yeye, msanii mwingine aliyecheza nafasi ya mwanakwaya naye alipoteza fahamu wakati kipande hicho kikirekodiwa.
TATIZO UHALISIA, WASIWASI
Chanzo kimoja kutoka ndani ya kundi la wasanii waliokuwa wakiigiza filamu kinasema kuwa, Chuchu alikumbwa na hali hiyo kutokana na wasiwasi na ujasiri wa kuuvaa uhusika.
“Awali, Chuchu alionesha wasiwasi wa kuigiza kipande hicho cha kumwonesha yeye yumo ndani ya jeneza akiwa amefariki dunia kwa ugonjwa kama wa kichaa kilichotokana na msongo wa mawazo baada ya kubakwa.
“Mbaya zaidi, mwongozaji naye alisema ni lazima akiwa amelala ndani ya jeneza awekewe pamba za kuziba matundu ya pua kama maiti wanavyowekewa,” kilisema chanzo.
...Waombolezaji wakilia kwa uchungu.
ILIKUWA WAKATI AKIAGWA
Chanzo kikazidi kudai kwamba, taharuki yote hiyo ilitokea pale, ‘mwili’ wa Chuchu ukiagwa kwenye Kanisa la Sabato, Mbezi, Dar ambapo waombolezaji walipokuwa wakipita, binti yake, Farha (9) aliangua kilio kilichomfanya Chuchu ajikute akikata pumzi ghafla!
AMALIZA SINI, ASHINDWA KUAMKA
Ikaelezwa kwamba, ilikuwa wakati kipande hicho kimeisha huku binti yake akiendelea kulia kwa kumwona mama yake ndani ya jeneza, Chuchu hakuamka ili kuendelea na vipande vingine hali iliyowafanya watu wazima kumkagua na kugundua alizirai.
“Watu walianza kupagawa, wengine walijua ameshapoteza maisha. Lakini Mungu mkubwa Chuchu akazinduka na kumkuta mwanaye bado akilia kwa nguvu. Ilibidi wasanii wengine waingilie kati kumtuliza,” kilisema chanzo.
Waombolezaji wakiwa na simanzi.
MWINGINE AITIWA MCHUNGAJI
Wakati Chuchu ‘akifufuka’, yule msanii aliyeigiza nafasi ya mwanakwaya yeye alikuwa bado chini amelala chali akiwa hajitambui kwa kile kilichokuwa kikiendelea.“Yule mwenzake ilibidi aitwe mchungaji wa kanisa hilo ambaye alikuwa jirani kwa ajili ya kumwombea japo mchungaji wa filamu hiyo alikuwa ni msanii Jimy Mafufu,” kilisema chanzo.
MASWALI ENEO LA TUKIO
Baadhi ya wasanii walianza kujiuliza nini kilisababisha hali ile kwani ilionekana kama kuna roho chafu aliyetaka kufanya mauaji ya makusudi.
“Wengine waliuliza kama kuna mtu ana vitu kama hirizi au chanjo ya mambo ya kishirikina, ikaonekana hakuna. Lakini maswali yalikuwa mengi sana,” kilisema chanzo.

Jeneza likiandaliwa kwa ajili ya mazishi.
CHUCHU AONGEA NA AMANI
Baada ya kuinasa taarifa hiyo, Amani lilimsaka Chuchu kwa njia ya simu yake ya mkononi na kumuuliza ambapo alikiri kutokea kwa tukio hilo.
Huyu hapa:  “Yaani siwezi kueleza juu ya ile filamu maana ilikuwa ni hatari tupu na sijui hata mama yangu akiiona itakuaje kwa kweli.
“Lakini kwenye ile sini yangu ndiyo ilikuwa ikihitaji hivyo, nilale kama maiti kweli na huwezi amini lilichimbwa hadi kaburi la ukweli. Mimi nilizimia si chini ya  mara moja. Pumzi yangu ilikata hasa nilipomsikia mwanangu akilia.”
CHUCHU ANAWEZA ASIWE SAWA KISAIKOLOJIA
Kwa mujibu wa maswali ya kisaikolojia kwa wasanii wa maigizo, baada ya msanii kuigiza filamu inayohusu ukatili wowote, kumwaga damu, mapenzi ya kupitiliza, kifo au jambo lolote ambalo ni chungu kwa ubinadamu ni lazima aombewe na viongozi wa dini ili kuifukuza roho hiyo ya kuigizia.
Wanasaikolojia wanasema kuwa, msanii akiigiza nafasi kama hizo na kujiacha hivihihivi kuna hatari baada ya muda kuambukizwa na uigizaji huo ikawa ndiyo maisha yake ya kila siku. Ndiyo maana baadhi ya wasanii wa filamu duniani kote wanaishi maisha ya sawasawa na wanavyocheza filamu.